1Mimi nitasimama pahali pa kuchungulia,
na kuikaa juu katika munara;
nitakaa macho wazi nipate kuona ataniambia nini,
atajibu nini juu ya malalamiko yangu.
Mungu anamujibu Habakuki2Kisha, Yawe akanijibu hivi:
Uyaandike maono haya;
uyaandike wazi juu ya vibao,
anayepitia pale apate kuyasoma haraka.
3Maono haya yanangoja wakati uliopangwa;
ni maono ya ukweli juu ya mwisho.
Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee;
hakika yatafika, wala hayatachelewa.
4Andika:
Uwaangalie wenye kiburi, hao wataangamia;
lakini wenye haki wataishi kwa kumwamini Mungu. Waovu wataangamia
5Zaidi ya hayo, divai inapotosha;
mutu mwenye kiburi hatadumu.
Yuko tayari kuwameza wengine kama kuzimu;
kama vile kifo, hatosheki na kitu.
Anajikusanyia mataifa yote,
na watu wote kama mali yake.
6Kila mutu atamuchekelea mutu wa namna hiyo
na kumutungia misemo ya kitambi:
Ole wako unayejilundikia visivyokuwa vyako,
na kutwaa rehani mali za watu lakini haulipi!
Utaendelea kufanya hivyo mpaka wakati gani?
7Siku moja wale waliokukopesha watasimama kwa rafla,
wale wanaokutetemesha wataamuka.
Halafu utakuwa mateka wao.
8Wewe umenyanganya mataifa mengi,
lakini wote wanaobaki watakunyanganya wewe,
kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia,
uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.
9Ole wako unayejitajirisha kwa hasara ya mwingine,
unayejenga nyumba yako juu katika milima
ukizani kuwa salama mbali na hasara.
10Lakini kwa mipango yako umefezehesha jamaa lako.
Kwa kuyaangamiza mataifa mengi,
umeyaangamiza maisha yako mwenyewe.
11Ndiyo maana hata mawe yatalalamika juu ya ukuta,
na miti ya nyumba itayaunga mukono.
12Ole wako unayejenga muji kwa mauaji
unayesimika kijiji kwa maovu!
13Yawe wa majeshi anasababisha
juhudi za watu zipotelee katika moto,
na mataifa yajishugulishe bure.
14Utukufu wa Yawe utaenea pote katika dunia,
kama vile maji yanavyoenea katika bahari.
15Ole wako unayewalewesha jirani zako,
na kutia sumu katika divai yao
kusudi upate kuwaona wakiikaa uchi.
16Utajaa haya pahali pa heshima.
Utakunywa wewe mwenyewe na kupepesuka!
Yawe mwenyewe atakulewesha,
na haya itaifunika heshima yako!
17Mateso uliyoyatenda kule Lebanoni yatakulemea wewe;
uliwaua nyama, nyama nao watakuogopesha.
Yote hayo yatakupata wewe,
kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia,
uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.
18Sanamu mutu aliyotengeneza inafaa kwa nini?
Sanamu ni madini yaliyoyeyushwa,
ni kitu cha kueneza udanganyifu!
Mutengenezaji wa sanamu anatumainia kile alichotengeneza mwenyewe,
sanamu ambayo haiwezi hata kusema!
19Ole wake mutu anayeambia kipande cha muti: Amuka!
au jiwe bubu: Simama!
Sanamu inaweza kumufundisha mutu?
Angalia imepakwa zahabu na feza,
lakini haina uzima wowote.
20Lakini Yawe yuko katika hekalu lake takatifu;
dunia yote ikae kimya mbele yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.