1Basi, Rehoboamu akaenda Sekemu ambako Waisraeli wote walikuwa wamekusanyika kwa kumuweka kuwa mufalme.
2Naye Yeroboamu mwana wa Nebati alipopata habari juu ya tendo hilo, maana alikuwa angali Misri ambako alikwenda alipomukimbia Solomono, alirudi kutoka Misri.
3Kisha Waisraeli walituma ujumbe na kumwita. Basi, yeye pamoja na Waisraeli hao wote walimwendea Rehoboamu, wakamwambia:
4“Baba yako alitubebesha muzigo muzito. Basi, utupunguzie muzigo huo muzito wa baba yako, nasi tutakutumikia.”
5Naye Rehoboamu akawaambia: “Mwende, murudie kwangu kesho kutwa.”
Basi, wakaondoka.
6Nyuma Rehoboamu alitaka kujua maoni ya wazee ambao walikuwa washauri wa baba yake Solomono alipokuwa angali muzima, akawauliza: “Munanishauria niwape jibu gani watu hawa?”
7Wazee hao wakamujibu: “Leo ukiwa mutumishi wa watu hawa, ukiwatumikia na kuongea nao vizuri unapowajibu, pale watakuwa watumishi wako siku zote.”
8Lakini Rehoboamu alizarau shauri la wazee. Pahali pa shauri lile akashauriana na vijana waliokomaa pamoja naye ambao walikuwa washauri wake.
9Basi, akawauliza: “Ninyi munatoa shauri gani kusudi tuweze kuwajibu watu hawa walioniambia niwapunguzie muzigo ambao baba yangu aliwabebesha?”
10Hao vijana wakamujibu: “Watu hao waliokuambia baba yako aliwabebesha muzigo muzito, wakakuomba uwapunguzie muzigo ule, wewe uwaambie hivi: ‘Kidole changu kidogo cha mwisho ni kinene zaidi kuliko kiuno cha baba yangu.
11Muzigo wa baba yangu ulikuwa muzito, lakini wangu utakuwa muzito zaidi. Baba yangu aliwapiga ninyi kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba.’ ”
12Basi, siku ya tatu Yeroboamu pamoja na watu wote wakarudi kwa Rehoboamu kama alivyokuwa amewaagiza.
13Mufalme akawajibu watu hao kwa ukali, akazarau shauri alilopewa na wazee,
14akafuata shauri la vijana wenzake, akawaambia: “Baba yangu aliwabebesha muzigo muzito, lakini mimi nitaufanya kuwa muzito zaidi. Baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba.”
15Hivyo, mufalme hakuwajali watu kwa sababu jambo hili lilisababishwa na Yawe, kusudi atimize neno lake alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati, kwa njia ya Ahiya wa Shilo.
16Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mufalme hakuwajali, walimwambia:
“Hatuna ushirika wowote na Daudi!
Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese.
Murudie kwenu, enyi watu wa Israeli!
Uitunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.”
Hivyo, watu wa Israeli wakarudi kila mutu kwake.
17Watu wa Israeli waliokuwa wanakaa katika miji ya Yuda, ndio hao tu waliobaki chini ya utawala wa Rehoboamu.
18Mufalme Rehoboamu alipomutuma Adoramu, aliyekuwa musimamizi mukubwa wa kazi za kulazimishwa, watu wote wa Israeli walimutupia mawe, wakamwua. Naye Rehoboamu alipanda haraka ndani ya gari lake, akakimbilia Yerusalema.
19Hivyo watu wa Israeli wakakuwa katika hali ya uasi mbele ya ukoo wa Daudi mpaka leo.
20Watu wote wa Israeli walipopata habari kwamba Yeroboamu alikuwa amerudi kutoka Misri, walimwita katika mukutano, wakamuweka kuwa mufalme wa Israeli yote. Hakuna kabila lingine lililojiunga na ukoo wa Daudi isipokuwa tu kabila la Yuda.
Unabii wa Semaya(2 Sik 11.1-4)21Rehoboamu alipofika Yerusalema, alikusanya waaskari wafundi wa vita elfu mia moja na makumi nane wa makabila ya Yuda na Benjamina, apate kupigana na utawala wa Israeli, kusudi aurudishe utawala kwa Rehoboamu mwana wa Solomono.
22Lakini ujumbe huu wa Mungu ulitolewa kwa Semaya, mutu wa Mungu:
23“Umwambie Rehoboamu mwana wa Solomono, mufalme wa Yuda, na watu wote wa kabila la Yuda na Benjamina na watu wengine,
24kwamba mimi Yawe ninasema hivi: ‘Musiende, wala musipigane na wandugu zenu, watu wa Israeli. Murudie kila mutu kwake, maana hayo yaliyotokea ni mupango wangu.’ ” Basi, wakaufuata ujumbe huu wa Yawe, wakarudi kwao tena kama vile Yawe alivyoagiza.
Yeroboamu anamwasi Yawe25Nyuma ya mambo hayo, mufalme Yeroboamu akaujenga upya muji wa Sekemu kwenye mulima wa Efuraimu. Akakaa kule. Kisha akaenda kujenga muji wa Penueli.
26Halafu Yeroboamu akaanza kufikirifikiri: “Sasa ufalme utarudi kwa jamaa ya mufalme Daudi
27kama watu hawa wataendelea kwenda kutoa sadaka katika nyumba ya Yawe kule Yerusalema. Mioyo yao itamugeukia bwana wao Rehoboamu mufalme wa Yuda, nao wataniua mimi.”
28Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”
29Akaiweka sanamu moja katika muji wa Beteli, na ya pili katika muji wa Dani.
30Tendo hili likakuwa zambi, maana watu waliandamana kwenda kuzitambikia sanamu hizo kule Beteli na Dani.
31Vilevile, Yeroboamu alijenga nafasi ya kutambikia juu ya vilima, akachagua makuhani ambao hawakukuwa wa ukoo wa Lawi.
32Yeroboamu aliamuru vilevile siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane ikuwe sikukuu sawa na ile sikukuu iliyokuwa inafanyika kule Yuda. Alitoa sadaka kwenye mazabahu aliyotengeneza kule Beteli mbele ya zile sanamu za wana-ngombe alizozitengeneza, akaweka wale makuhani aliowachagua watumike kila nafasi ya kutolea sadaka aliyotengeneza juu ya vilima.
33Siku hiyo ya kumi na tano ya mwezi wa nane, aliifanya yeye mwenyewe, naye akaenda Beteli kwa kutambikia. Ndivyo alivyoiimarisha sikukuu hiyo aliyoiweka kwa ajili ya watu wa Israeli, naye mwenyewe akapanda kuiendea mazabahu, kufukiza ubani.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.