Zaburi 80 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maombi kwa ajili ya taifa

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo. Zaburi ya Asafu.

2Unitegee sikio, ewe Muchungaji wa Israeli,

unayewaongoza wazao wa Yosefu kama kondoo.

Ewe unayekaa juu ya makerubi, uangaze,

3mbele ya kabila la Efuraimu, la Benjamina na la Manase.

Uonyeshe nguvu yako, ukuje kutuokoa!

4Utengeneze tena maisha yetu, ee Mungu;

utuangalie kwa wema, nasi tutaokoka.

5Ee Yawe, Mungu wa majeshi,

mpaka wakati gani utakasirikia maombi ya watu wako?

6Umefanya huzuni ikuwe chakula chetu;

umetukunywesha machozi kwa wingi.

7Umetufanya jambo la mazarau kwa jirani zetu;

waadui zetu wanatuchekelea.

8Ee Mungu wa majeshi, utengeneze tena maisha yetu,

utuangalie kwa wema, nasi tutaokoka.

9Uliongoa muzabibu kutoka Misri;

ukawafukuza watu wa mataifa,

na kuupandikiza katika inchi yao.

10Uliupalilia upate kukomaa,

nao ukatoa mizizi na kuenea katika inchi yote.

11Uliifunika milima kwa kivuli chake,

na matawi yake yakakuwa kama mierezi mikubwa.

12Matawi yake yalienea mpaka kwa bahari;

navyo vichipukizi vyake mpaka kando ya muto Furati.

13Mbona ulibomoa kuta zilizouzunguka?

Sasa kila anayepita anachuma zabibu zake;

14nguruwe wa mwitu wanauharibu,

na wanyama wa pori wanautafuna!

15Utugeukie tena, ee Mungu wa majeshi.

Uangalie toka mbinguni, uone;

uutunze muzabibu huu.

16Ulinde kijiti ulichokipanda kwa mukono wako;

hicho kichipukizi ulichokomalisha wewe mwenyewe.

17Watu walikikata na kukiteketeza,

uwaangalie kwa ukali, waangamie.

18Mukono wako umukinge huyo uliyemurehemu;

huyo uliyemuchagua kwa ajili yako.

19Hatutakuacha tena;

utujalie uzima, nasi tutakusifu.

20Ee Yawe, Mungu wa majeshi, utengeneze tena maisha yetu;

utuangalie kwa wema, nasi tutaokoka.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help