1Zaburi ya Daudi.
Ee Yawe,
ninakutolea moyo wangu.
2Ninakutumainia wewe, ee Mungu wangu,
usiniache nifezeheke;
waadui zangu wasifurahie kushindwa kwangu.
3Usimwache anayekutumainia kupata haya;
lakini wafezeheke wote wanaokuasi kwa makusudi.
4Unijulishe njia zako, ee Yawe;
unifundishe nifuate unayotaka.
5Uniongoze katika ukweli wako na kunifundisha,
kwa maana wewe ni Mungu, mwokozi wangu;
ninakutegemea wewe kila siku.
6Ee Yawe, ukumbuke
rehema yako na wema wako
ambazo ni za milele.
7Usikumbuke zambi na makosa ya ujana wangu;
unikumbuke kwa kadiri ya wema wako,
kwa ajili ya uzuri wako, ee Yawe.
8Yawe ni muzuri na wa usawa,
kwa hiyo anawafundisha wakosaji njia.
9Anawaongoza wanyenyekevu katika haki;
anawafundisha njia yake.
10Njia zote za Yawe ni njema na za uaminifu
kwa wale wanaoshika agano lake na maagizo yake.
11Kwa ajili ya jina lako, ee Yawe,
unisamehe kosa langu, kwa maana ni kubwa.
12Kila mutu anayemwabudu Yawe,
Yawe atamufundisha njia ya kufuata.
13Mutu wa namna hiyo atafanikiwa siku zote,
na wazao wake watarizi inchi.
14Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu;
yeye anawajulisha agano lake.
15Ninainua macho kwa Yawe siku zote;
yeye ataopoa miguu yangu kutoka mutego.
16Unielekee, ee Mungu, unionee huruma,
maana mimi ni pekee na zaifu.
17Uniondolee mahangaiko ya moyo wangu;
uniondoe katika mashaka yangu.
18Uangalie mateso yangu na taabu yangu;
unisamehe zambi zangu zote.
19Angalia jinsi waadui zangu wanavyokuwa wengi;
ona jinsi wanavyonichukia vikali.
20Uyalinde maisha yangu, uniokoe;
ninakukimbilia wewe, usikubali nifezeheke.
21Ukamilifu na usawa vinanikinga,
maana ninakutumainia wewe.
22Ee Mungu, uwaokoe watu wako, Israeli;
uwaokoe kutoka taabu zao zote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.