1Solomono alipomaliza maombi yake, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuchoma sadaka na sadaka za kuteketeza kwa moto zilizotolewa, kisha utukufu wa Yawe ukajaza nyumba.
2Makuhani hawakuweza kuingia mule kwa sababu utukufu wa Yawe ulijaa nyumba ya Yawe.
3Waisraeli wote walipoona moto ukishuka kutoka mbinguni na utukufu wa Yawe katika nyumba, wakainama nyuso zao zikifika mpaka chini. Wakamwabudu na kumushukuru Yawe wakisema:
“Yeye ni muzuri.
Wema wake unadumu milele.”
4Kisha mufalme Solomono na watu wote wakamutolea Yawe sadaka.
5Naye Solomono akamutolea ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja makumi mbili. Hivi ndivyo Solomono na watu wote walivyozinduwa nyumba ya Mungu.
6Makuhani walikuwa wakisimama kwenye nafasi za kazi zao, nao Walawi, walisimama wakiwa na vyombo vya Yawe vya muziki mufalme Daudi alivyotengeneza kwa ajili ya kutoa shukrani kwa Yawe. Waliimba: “Wema wake unadumu milele.” Wakati Daudi alipotoa shukrani, walimusaidia; makuhani walipiga baragumu nao Waisraeli wote wakasimama.
7Basi, mufalme Solomono akazindua sehemu ya katikati ya kiwanja kilichokuwa mbele ya nyumba ya Yawe, maana ni pale ndipo alipotolea sadaka za kuteketezwa kwa moto na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu ile mazabahu ya shaba haikutosha kwa sadaka zile zote.
8Naye Solomono kwa muda wa siku saba alifanya sikukuu pamoja na kusanyiko kubwa la watu wote wa Israeli waliotoka kwenye kiingilio cha Hamati mpaka kwenye muto wa Misri.
9Siku ya nane, walikusanyika wakafanya sikukuu nyuma ya muda wa siku saba, walizotumia kwa kutakasa meza ya matoleo ya sadaka, na siku saba nyingine za sikukuu.
10Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku ya makumi mbili na tatu ya mwezi wa saba, Solomono akawaaga watu waende kwao, wakishangilia na kufurahi ndani ya moyo kwa sababu ya mazuri ambayo Yawe alimutendea Daudi, Solomono na kwa watu wake Waisraeli.
Mungu anamutokea tena Solomono(1 Fal 9.1-9)11Basi, mufalme Solomono akamaliza kujenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme na kutimiza yale yote aliyokusudia kuifanyia nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme.
12Kisha Yawe akamutokea usiku, akamwambia: “Nimesikia maombi yako na nimechagua pahali hapa pakuwe nyumba yangu ya kunitolea sadaka.
13Nikiwanyima mvua au nikiwaletea nzige wakule mimea yao au nikiwapiga kwa ugonjwa mukali
14kama watu wangu hao wakijinyenyekeza, wakiomba, wakinitafuta na kuacha njia zao mbaya, basi, mimi nitawasikiliza kutokea juu mbinguni, nitawasamehe zambi yao na kustawisha inchi yao.
15Sasa nitachunga hekalu hili na kusikiliza maombi yatakayofanyika hapa,
16kwa maana nimetakasa nyumba hii kusudi watu waliabudu jina langu hapa milele. Nitailinda na kuipenda siku zote.
17Nawe kama ukinitumikia kwa uaminifu kama vile Daudi baba yako alivyofanya, ukitenda yote niliyokuamuru na kutii maongozi yangu na maagizo yangu,
18basi, mimi nitaimarisha kiti chako cha kifalme kama nilivyofanya agano na Daudi baba yako nikisema: ‘Hautakosa mutu wa kutawala inchi ya Israeli.’
19“Lakini mukiacha kunifuata, na kuasi maongozi yangu na amri nilizowapa, na kwenda kutumikia miungu mingine na kuiabudu,
20kwa sababu hiyo mimi nitawaongoa kutoka katika inchi hii ambayo nimewapa. Vielvile na nyumba hii ambayo nimeitakasa kwa ajili ya jina langu nitaitupilia mbali nami, na kuifanya kitu cha kuchekelewa na kuzarauliwa kati ya mataifa yote.”
21“Na juu ya nyumba hii ambayo nimetukuzwa, kila anayepita karibu atashituka na kuuliza: ‘Kwa nini Yawe amefanya hivyo kwa inchi hii na kwa nyumba hii?’
22Watu wengine watajibu: ‘Ni kwa sababu walimwacha Yawe, Mungu wa babu zao aliyewatoa toka katika inchi ya Misri; wakashikamana na miungu mingine, wakaiabudu na kuitumikia. Kwa hiyo Yawe amewaletea hasara hizi zote.’ ”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.