1-6Solomono alikuwa mufalme wa inchi yote ya Israeli, na hawa ndio walikuwa wakubwa wa serikali yake wenye vyeo vya juu:
Azariya mwana wa Zadoki alikuwa kuhani.
Elihorefu na Ahiya, wana wa Sisa, walikuwa wakatibu.
Yosafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwandishi wa habari.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa waaskari.
Zadoki na Abiatari walikuwa makuhani.
Azariya mwana wa Natani alikuwa mukubwa wa maliwali.
Kuhani Zabudi mwana wa Natani alikuwa rafiki ya mufalme.
Ahisari alikuwa mukubwa wa nyumba ya mufalme.
Adoniramu mwana wa Abuda alikuwa musimamizi wa kazi za kulazimishwa.
7Solomono alichagua maliwali kumi na wawili kwa inchi nzima ya Israeli. Hao walipewa kazi ya kutafuta chakula kwa ajili ya mufalme na nyumba yake. Kila mumoja wao alileta chakula kutoka jimbo lake kwa mwezi mumoja kila mwaka.
8-19Haya ndiyo majina ya hao maliwali:
Beni-Huri alisimamia sehemu ya milima ya Efuraimu.
Beni-Dekari alisimamia miji ya Makasi, Salabimu, Beti-Semesi na Eloni-Beti-Hanani.
Beni-Hesedi alisimamia muji wa Aruboti, alisimamia vilevile Soko na inchi yote ya Heferi.
Beni-Abinadabu, mume wa Tafati, binti ya Solomono, alisimamia jimbo lote la Dori.
Bana mwana wa Ahiludi, alisimamia miji ya Tanaki, Megido, na sehemu yote ya Beti-Seani inayokuwa karibu na muji wa Zaretana, upande wa kusini wa muji wa Yezereheli, na kutoka Beti-Seani mpaka miji ya Abeli-Mehola, na hata kupita muji wa Yokimamu.
Beni-Geberi alisimamia muji wa Ramoti-Gileadi pamoja na vijiji vya Gileadi vilivyokuwa vya Yairi mwana wa Manase; tena alisimamia jimbo la Argobu katika inchi ya Basani; yote kwa jumla ilikuwa miji mikubwa makumi sita iliyozungushiwa kuta na kuwekwa vifungio vya shaba kwenye mulango.
Ahinadabu mwana wa Ido, alisimamia jimbo la Mahanaimu.
Ahimasi, mume wa Basemati, binti ya Solomono, alisimamia sehemu ya inchi ya Nafutali.
Bana mwana wa Husayi, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Aseri na Bealoti.
Yosafati mwana wa Parua, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Isakari.
Simei mwana wa Ela, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Benjamina.
Geberi mwana wa Uri, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Gileadi, ambayo zamani ilitwaliwa na Sihoni mufalme wa Waamori, na Ogu mufalme wa Basani.
Zaidi ya hawa kumi na wawili, kulikuwa mukubwa mumoja aliyesimamia inchi nzima ya Yuda.
Utawala wa Solomono unafanikiwa20Watu wa Yuda na wa Israeli walikuwa wengi kama muchanga wa bahari, nao walikuwa wakikula, wakikunywa, na kufurahi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.