Yobu 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Sehemu ya kwanza ya Mazungumuzo(4.1–14.22)Masemi ya Elifasi

1Kisha Elifasi wa inchi ya Temani akamujibu Yobu:

2Mutu akijaribu kukuambia neno utakasirika?

Lakini nani anayeweza kujizuia kusema?

3Sikiliza! Wewe umewafundisha wengi,

na kuiimarisha mikono ya wazaifu.

4Maneno yako yamewainua moyo,

umewaimarisha waliokosa nguvu.

5Lakini sasa shida imekupata nawe unaregea.

Imekugusa, nawe unafazaika.

6Kumwogopa Mungu si ndilo tegemeo lako?

Na ukamilifu wa mwenendo wako si ndilo tumaini lako?

7Fikiri sasa: nani asiyekuwa na kosa ambaye amepata kuangamia?

Au, watu wa usawa wamepata kutupiliwa?

8Mimi nimeona kwamba wanaopanda uovu na ubaya wanavuna yaleyale.

9Mungu anawaangamiza kwa pumzi yake;

wanateketezwa kwa kuvuma kwa hasira yake.

10Waovu wananguruma kama simba mukali,

lakini meno yao inavunjwa.

11Simba mwenye nguvu anakufa kwa kukosa chakula,

na watoto wa simba dike wanatawanywa!

12Siku moja, niliambiwa neno kwa siri,

sikio langu lilisikia manongonezo yake.

13Ilikuwa usiku wakati watu wanapoota ndoto,

wakati usingizi muzito unawashika watu.

14Nikashikwa na hofu na kutetemeka;

mifupa yangu yote ikagonganagongana.

15Upepo ukapita mbele ya uso wangu,

nywele za mwili wangu zikasimama.

16Kitu kimoja kikasimama mbele yangu.

Nilipokiangalia sikukitambua kabisa.

Kulikuwa umbo moja mbele yangu.

Kulikuwa kimya, kisha nikasikia sauti:

17“Mwanadamu anaweza kuwa mwenye haki mbele ya Mungu?

Mutu anaweza kuwa safi mbele ya Muumba wake?

18Mungu hawaaminie hata watumishi wake,

na wamalaika wake anawaona wana kosa.

19Zaidi sana wanadamu,

viumbe vya udongo,

watu ambao musingi wao ni mavumbi,

ambao wanaweza kupondwapondwa kama chawa!

20Wanadamu wanaangamia kwa saa chache tu;

wanaangamia milele bila kuacha hata alama.

21Kama uzi unaoshikilia uzima wao ukikatwa,

wao wanakufa, tena bila kuwa na hekima”.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help