Yobu 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Halafu Bildadi wa inchi ya Suhi akamujibu Yobu:

2Utasema mambo haya mpaka wakati gani?

Mpaka wakati gani maneno yako yatakuwa matupu kama upepo?

3Maana, unazani Mungu anapotosha sheria?

Au, Mungu Mwenye Uwezo anapotosha haki?

4Kama watoto wako wamemukosea Mungu,

yeye amewalipiza matokeo ya makosa yao.

5Kama utamutafuta Mungu

na kumusihi yule Mungu Mwenye Uwezo,

6kama wewe uko safi ndani ya moyo na wa usawa,

kweli Mungu atakuja kukusaidia,

na kukujalia makao unayostahili.

7Na ingawa ulianza kuishi kwa uzaifu,

maisha yako ya mwisho yatakuwa bora zaidi.

8Tafazali, ujifunze kwa wale waliotutangulia;

shika mambo ambayo wazee walitambua.

9Sisi ni watu wa juzijuzi tu, hatujui kitu;

siku zetu katika dunia ni kivuli kinachopita.

10Lakini wao watakufundisha na kukuambia

mambo waliyopata kuyatoa katika maarifa yao.

11Nyasi zinaota tu penye tingitingi,

matete yanastawi pahali panapokuwa maji.

12Hata kama yamechanua na bila kukatwa,

yakikosa maji yananyauka mbele ya mimea mingine.

13Ndivyo wote wanaomusahau Mungu wanavyokuwa.

Tumaini la wasiomwamini Mungu litapotea.

14Tegemeo lao linavunjika,

tumaini lao ni utando wa buibui.

15Wanaegemea nyumba yao lakini haitasimama,

wanaishikilia lakini haidumu.

16Wako kama ua ambalo jua linapotoka linastawi;

linaeneza matawi yake katika bustani yake,

17mizizi yake inajisokotasokota kwenye mawe,

nalo linaenda kuchunguza ndani ya jiwe.

18Lakini likiangamizwa kutoka makao yake,

hayo yatalikana yakisema: “Sijakuona bado.”

19Ile ndiyo furaha ya mwisho wake,

na pahali pake patachipuka mengine.

20Sikia! Mungu hatakataa mutu mukamilifu,

wala hatasaidia waovu.

21Lakini atajaza kinywa chako kicheko,

na midomo yako sauti ya furaha.

22Wale wanaokuchukia watapata haya,

makao ya waovu yatatoweka kabisa.

Jibu la Yobu
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help