1Roho wa Mungu alimujaza Azaria mwana wa Obedi,
2naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.
3Kwa muda murefu sasa, Waisraeli wameishi bila Mungu wa kweli, wala makuhani wa kuwafundisha, na bila Sheria.
4Lakini walipopatwa na shida, walimugeukia Yawe, Mungu wa Israeli, wakamutafuta, wakamupata.
5Katika siku zile, hakuna mutu aliyeweza kuingia wala kutoka kwa usalama kwa sababu hapakukuwa amani; fujo nyingi sana ziliwasumbua wanainchi wa kila inchi.
6Taifa moja lilipigana na taifa lingine na muji mumoja ulipigana na muji mwingine, kwa sababu Mungu aliwafazaisha kwa taabu za kila aina.
7Lakini ninyi mujipe moyo, wala musiregee kwa maana mutapata malipo kwa kazi munayofanya.”
8Asa aliposikia maneno haya, ni kusema unabii wa Azaria mwana wa Odedi, yakamutia moyo. Akaondoa sanamu zote za kuchukiza katika inchi yote ya Yuda na ya Benjamina, na kutoka katika miji yote aliyoteka katika inchi ya milima ya Efuraimu. Na kisha akatengeneza upya mazabahu ya Yawe iliyokuwa katika baraza la nyumba ya Yawe.
9Asa akakusanya watu wote wa Yuda na Benjamina, na wengine wote waliokuwa wakikaa katika inchi yake kutoka kabila la Efuraimu, la Manase na la Simeoni. Hawa walikuja kwake walipoona kwamba Yawe, Mungu wake yuko pamoja naye.
10Wote walikusanyika Yerusalema katika mwezi wa tatu wa mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
11Siku ile, walimutolea Yawe sadaka za ngombe mia saba na kondoo elfu saba, kutoka katika vile vitu walivyoteka.
12Nao wakafanya agano, kwamba watamutafuta Yawe, Mungu wa babu zao, kwa moyo wote na kwa roho yao yote;
13na kwamba yeyote asiyemutafuta Yawe, Mungu wa Israeli, akuwe kijana au muzee, mwanaume au mwanamuke, sharti auawe.
14Walimwapia Yawe kwa sauti kubwa, wakalalamika zaidi, wakapiga ngunga na baragumu.
15Watu wote wa Yuda walikuwa na furaha tele kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wote. Walikuwa wamemutafuta kwa hamu, wakamupata. Naye Yawe akawapa amani pande zote.
16Mufalme Asa alimwondoa hata mama yake Maka, cheo chake cha malkia, kwa sababu alitengeneza sanamu ya kuchukiza ya Ashera, mungu wa kike. Asa alikatakata sanamu hiyo, akaipondaponda na kuiteketeza kwa moto katika bonde la kijito Kidroni.
17Lakini hata hivyo pahali pa kutambikia miungu mingine katika Israeli hapakuharibiwa; lakini yeye alikuwa na moyo mwaminifu maisha yake yote.
18Alivirudisha katika nyumba ya Mungu vifaa vyote vilivyotakaswa na baba yake pamoja na vile alivyotakasa yeye mwenyewe; feza na zahabu na vyombo vingine.
19Hapakukuwa vita tena katika inchi mpaka mwaka wa makumi tatu na tano wa utawala wa Asa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.