1Kisha Yobu akajibu:
2Musikilize kwa uangalifu maneno yangu;
na hiyo ikuwe ndiyo faraja yenu.
3Munivumilie, nami nitasema,
na nikisha sema muendelee kunichekelea.
4Basi, mimi ninamulalamikia mwanadamu?
Kwa nini basi nikose uvumilivu?
5Muniangalie, nanyi mushangae,
muweke mikono yenu juu ya vinywa vyenu.
6Nikifikiri yaliyonipata ninafazaika,
mwili wangu unatetemeka kwa hofu.
7Kwa nini waovu wanaendelea kuishi?
Mbona nguvu zao zinaongezeka hata katika uzee?
8Wanaona watoto wao wakifanikiwa
na wazao wao wakipata nguvu.
9Kwao kila kitu ni salama bila hofu,
wala fimbo ya Mungu haiwafikii.
10Kweli, ngombe wao wote wanaongezeka,
wanazaa bila matatizo yoyote.
11Watoto wao wachanga wanatembea kama kundi;
na watoto wao wanacheza ngoma;
12wanacheza muziki wa ngoma na vinubi,
na kufurahia sauti ya filimbi.
13Wanaishi maisha ya fanaka
kisha wanashuka kwa amani katika kuzimu.
14Wanamwambia Mungu: “Usitusumbue!
Hatutaki kujua mapenzi yako.
15Mungu Mwenye Uwezo ni nini hata tumutumikie?
Tunapata faida gani tukimwomba?”
16Kufanikiwa kwao si kuko katika mikono yao,
wakiwa wamemuweka Mungu mbali na mipango yao?
17Mara ngapi umepata kuona mwangaza wa maisha ya mwovu umezimishwa na kupatwa na hasara?
Au Mungu amekwisha kuwaangamiza kwa hasira yake?
18Hata hivyo, wapeperushwe kama majani yenye kukauka,
wakuwe kama maganda yanayopelekwa na zoruba!
19Ninyi munasema: “Mungu amewawekea watoto wao
azabu ya watu wale waovu.”
Kwa nini hawalipizi wao wenyewe, wapate kutambua?
20Waone wenyewe maangamizi yao;
waone wenyewe kasirani ya Mungu Mwenye Uwezo.
21Maana siku zao zitakapokwisha,
watajali nini juu ya wazao wao?
22Mwanadamu anaweza kumufundisha Mungu maarifa,
Mungu ambaye anahukumu wakaaji wa mbinguni?
23Mutu mumoja anakufa mwenye nguvu tele,
akiwa katika raha na salama,
24akijaa mafuta tele katika mwili,
na mifupa yake ikiwa bado na nguvu.
25Mwingine anakufa na huzuni kubwa ndani ya moyo,
akiwa hajaonja bado jambo lolote jema.
26Hata hivyo, wote wanakufa na kuzikwa,
wote wanafunikwa na vidudu.
27Musikilize! Mimi ninajua mawazo yenu yote,
na mipango yenu ya kunizarau.
28Ninyi munauliza: “Iko wapi nyumba ya yule mukubwa?
Iko wapi nyumba mwovu alimoishi?”
29Hamujawauliza wapita njia?
Hamukufahamu habari zao?
30Mwovu anaponyeshwa siku ya hasara,
anaokolewa siku ya kasirani!
31Ni nani atakayemwonyesha makosa yake,
au atakayemulipa kwa yote aliyotenda?
32Anapokamatwa kupelekwa katika kaburi,
kaburi lake linalindwa.
33Nyuma yake watu wengi wanamusindikiza
na wengine wengi sana wanamutangulia.
Anapozikwa, udongo unateremushwa polepole.
34Mutaweza namna gani basi, kunifariji kwa maneno matupu?
Majibu yenu hayana kitu chochote lakini uongo tu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.