Matayo 19 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mafundisho ya Yesu juu ya kuvunja ndoa(Mk 10.1-12)

1Yesu alipomaliza kusema maneno hayo akaondoka Galilaya. Akaenda katika jimbo la Yudea na kuvuka ngambo ya Yordani.

2Na makundi mengi ya watu wakamufuata, naye akawaponyesha wagonjwa kule.

3Wafarisayo wamoja wakamufikia kwa kumupima, wakamwuliza: “Sheria yetu inamuruhusu mutu kumufukuza muke wake haizuru kwa sababu gani?”

4Yesu akajibu: “Hamujasoma bado maneno yanayoandikwa katika Maandiko Matakatifu? ‘Kwa mwanzo Muumba aliumba mwanaume na mwanamuke,’

5na kisha akasema: ‘Kwa sababu hii, mutu atawaacha baba yake na mama yake na kuungana na muke wake, nao wawili watakuwa mwili mumoja.’

6Hivi wao si wawili tena, lakini wanakuwa mumoja. Basi mutu asitenganishe kile Mungu alichokiunganisha.”

7Halafu Wafarisayo wakamwuliza: “Kwa sababu gani basi Musa aliamuru kuandika barua ya kuachana wakati wa kumufukuza mwanamuke?”

8Yesu akawajibu: “Musa aliwapa ninyi ruhusa ya kuachana na wake wenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini haikuamuriwa vile tangu mwanzo.

9Na sasa mimi ninawaambia: kila mutu anayeachana na muke wake, isipokuwa kwa sababu ya uzinzi tu, na kumwoa muke mwingine, anazini.”

10Wanafunzi wake wakamwambia: “Ikiwa hayo ndiyo mapaswa ya mume kwa muke, hakuna mafaa ya kuoa.”

11Yesu akawajibu: “Si watu wote wanaoweza kukubali neno hilo munalosema, isipokuwa tu wale wanaojaliwa na Mungu.

12Kulingana na hayo, watu wamoja hawawezi kuoa kwa sababu walizaliwa towashi, wengine wamefanywa kuwa towashi na watu, wengine wamejifanya vile wenyewe kwa sababu ya kutumikia Ufalme wa mbinguni. Anayeweza kukubali mafundisho haya, ayakubali!”

Yesu anabariki watoto(Mk 10.13-16; Lk 18.15-17)

13Watu wamoja walimuletea Yesu watoto kusudi awawekee mikono na kuwaombea, lakini wanafunzi wakawakaripia watu wale.

14Lakini Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.”

15Naye alipokwisha kuweka mikono juu yao, akaondoka pale.

Kijana aliyekuwa tajiri(Mk 10.17-31; Lk 18.18-30)

16Kijana mumoja akamufikia Yesu na kumwuliza: “Mwalimu, nifanye jambo gani jema kusudi nipate uzima wa milele?”

17Yesu akamujibu: “Sababu gani unaniuliza juu ya jambo linalokuwa jema? Kuna mumoja tu anayekuwa mwema. Kama ukitaka kuingia pahali utakapopata uzima wa kweli, utii amri za Mungu.”

18Naye akauliza: “Amri gani?”

Yesu akamujibu: “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,

19uwaheshimu baba yako na mama yako na kumupenda mwenzako sawa wewe mwenyewe.”

20Yule kijana akamwambia: “Nimetii hizo amri zote. Ninakosewa na nini tena?”

21Yesu akamujibu: “Ukitaka kuwa mutimilifu, kwenda uuzishe vitu unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate.”

22Lakini yule kijana aliposikia maneno hayo, akajiendea akihuzunika, kwa sababu alikuwa tajiri sana.

23Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kweli ninawaambia: ni vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.

24Ninawaambia tena: ni kwepesi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

25Wanafunzi waliposikia maneno haya, wakashangaa sana na kuuliza: “Ni nani basi anayeweza kuokolewa?”

26Yesu akawaangalia na kuwaambia: “Jambo hilo haliwezi kutendeka kwa uwezo wa mwanadamu, lakini kwa uwezo wa Mungu, yote yanawezekana.”

27Halafu Petro akamwuliza: “Angalia, sisi tumeacha vyote na kukufuata wewe! Basi na sisi tutapata nini?”

28Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: Katika ulimwengu mupya, Mwana wa Mutu atakapoikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu, ninyi kumi na wawili mulionifuata mutaikaa vilevile juu ya viti kumi na viwili vya kifalme kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.

29Na kila mutu aliyeacha nyumba yake, kaka, dada, baba, mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara nyingi zaidi na kupewa uzima wa milele.

30Lakini wengi wanaokuwa wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wengi wanaokuwa wa mwisho watakuwa wa kwanza.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help