1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Kristo Yesu, niliyeitwa na Mungu kuwa mutume na niliyewekwa kwa kazi ya kutangaza Habari Njema yake.
2Habari Njema hiyo iliahidiwa na Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake katika Maandiko Matakatifu.
3-4Habari hiyo inaelekea Mwana wake ndiye Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye alizaliwa kimwili katika uzao wa mufalme Daudi. Lakini kwa namna ya Roho Mutakatifu, alihakikishwa kwa uwezo kuwa yeye ni Mwana wa Mungu kwa njia ya kufufuka kwake.
5Kwa njia yake Mungu amenipa neema ya kuwa mutume kusudi niongoze mataifa yote yapate kumwamini na kumutii. Na kwa tendo hilo jina lake lipate kusifiwa.
6Nanyi vilevile munakuwa kati ya watu wale; mumeitwa na Mungu mukuwe watu wa Yesu Kristo.
7Ninawaandikia ninyi wote wapenzi wa Mungu munaokaa Roma, mulioitwa kuwa watu wake watakatifu. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Paulo anatamani kuonana na Wakristo wa Roma8Kwanza ninamushukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu habari za imani yenu zinasambaa katika dunia nzima.
9Mungu ambaye ninamwabudu kwa roho yangu yote kwa njia ya kutangaza Habari Njema ya Mwana wake, ni mushuhuda wangu kwamba ninawakumbuka siku zote
10katika maombi yangu. Ninaomba kwamba Mungu akitaka, anifungulie njia ya kuwatembelea siku hizi.
11Kwa maana ninatamani sana kuonana nanyi, kusudi nigawanye pamoja nanyi zawadi ya kiroho, mupate kusimama imara.
12Ni kusema kwamba nipate kutiwa moyo kwa njia ya imani yenu na ninyi kwa njia ya imani yangu.
13Wandugu zangu, ninataka mujue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembelea, lakini mpaka sasa ninapata vizuizo. Ningetamani kupata matunda ya kazi yangu katikati yenu vilevile, kama inavyokuwa katikati ya watu wa mataifa mengine.
14Kwa sababu ninapaswa kwanza kuwaendea watu wote: Wagriki na wasiokuwa Wagriki, wenye elimu na wasiokuwa na elimu.
15Ni kwa sababu hii ninatamani sana kuhubiri vilevile Habari Njema kwenu ninyi munaokaa Roma.
Uwezo wa Habari Njema16Mimi sisikii haya juu ya Habari Njema, kwa sababu huo ndio uwezo wa Mungu unaowaokoa wote wanaoamini, kwanza Wayuda na kisha watu wa mataifa mengine vilevile.
17Kwa maana Habari Njema inaonyesha namna Mungu anavyowahesabia watu haki mbele yake. Jambo hilo haliwezekani isipokuwa kwa njia ya kuamini tu. Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yanayosema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”
Watu ni wenye zambi18Tokea mbinguni Mungu anaonyesha kwamba anawakasirikia wote wanaofanya zambi na maovu, wanaowazuiza watu wasitambue ukweli kwa njia ya matendo yao mabaya.
19Kwa maana mambo yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao, kwa kuwa Mungu mwenyewe ameyaonyesha kwao waziwazi.
20Tangu Mungu alipoumba dunia, hali zake zisizoonekana, ni kusema uwezo wake wa milele na umungu wake, vinaonekana kupitia viumbe vyake. Kwa sababu hii watu wale hawatapata namna yoyote ya kujitetea.
21Ijapokuwa wanamujua Mungu, hawamutukuzi wala kumushukuru kama vile anavyostahili. Lakini mawazo yao yaligeukia mambo ya ovyo ovyo, na mioyo yao isiyokuwa na ufahamu ilibaki katika giza.
22Wanajidai kwamba wao ni wenye hekima, lakini wako wapumbafu.
23Kwa pahali pa kumwabudu Mungu anayeishi milele, wakaabudu sanamu zilizochongwa kwa mufano wa mutu anayekufa, wa ndege, wa nyama na hata viumbe vyenye kutambaa.
24Kwa sababu hii Mungu aliwaacha wajichafue wenyewe kwa kufuata tamaa ya mioyo yao na kutendeana mambo ya haya wao kwa wao.
25Wanabadilisha ukweli juu ya Mungu kuwa uongo; wanaabudu na kutumikia vitu vilivyoumbwa kuliko Muumba mwenyewe, anayestahili kutukuzwa milele! Amina.
26Kwa hiyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za haya. Wanawake wao wanabadilisha matumizi ya kawaida na matumizi isiyokuwa ya kawaida.
27Na wanaume nao vilevile wanabadilisha matumizi ya kawaida ya mume na muke, wakiwakiana tamaa wanaume kwa wanaume. Kwa ajili ya hiyo, wanajipatia wenyewe azabu wanayoistahili kufuatana na huo upotevu wao.
28Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.
29Wamejaa kila namna ya uovu, ubaya, tamaa na upotovu. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na ukorofi. Wao ni wenye kuchongeana,
30wasingiziaji, wenye kumuchukia Mungu, wenye kasirani, wenye kiburi na wenye kujivuna. Wao ni werevu kwa kutenda mabaya, hawatii wazazi wao,
31hawana zamiri, hawawezi kuaminiwa, hawana upendo wala huruma.
32Nao wanajua kwamba Sheria ya Mungu inasema kwamba watu wanaotenda maneno haya wanastahili kufa. Lakini hata hivi wanaendelea, si kuyafanya tu, lakini kukubaliana na wale wanaoyatenda.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.