1 Mambo ya Siku 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wazao wa Yuda

1Wana wa Israeli walikuwa: Rubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuluni,

2Dani, Yosefu, Benjamina, Nafutali, Gadi na Aseri.

3-4Wana wa Yuda walikuwa watano: Wana wa Yuda aliozaliwa na Beti-Sua, muke wake Mukanana, walikuwa: Eri, Onanu na Sela. Eri, muzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Yawe, basi Yawe akamwua.

Na Tamari, muke wake alimuzalia wana wawili: Peresi na Zera.

5Wana wa Peresi walikuwa: Hesironi na Hamuli.

6Wana wa Zera walikuwa watano: Simuri, Etani, Hemanu, Kalkoli na Dara.

7Mwana wa Karmi alikuwa: Akana, ni kusema “Taabu”. Huyu aliwaletea Waisraeli taabu kwa sababu alijiwekea vitu vilivyolaaniwa.

8Mwana wa Etani alikuwa: Azaria.

9Wana wa Hesironi walikuwa: Yerameli, Ramu na Kelubai.

10-12Ramu alizaa Aminadabu,

Aminadabu alizaa Nasoni, mukubwa wa kabila la Yuda.

Nasoni alizaa Salma,

Salma alizaa Boazi,

Boazi alizaa Obedi,

Obedi alizaa Yese.

13Yese alizaa: Eliabu, muzaliwa wake wa kwanza, wa pili Abinadabu, wa tatu Simea,

14wa ine Netaneli, wa tano Radai,

15wa sita Osemu na wa saba Daudi.

16Wadada zao walikuwa Zeruya na Abigaili. Wana wa Zeruya walikuwa watatu: Abisai, Yoabu na Asaheli.

17Abigaili alikuwa baba ya Amasa ambaye baba yake alikuwa Yeteri, Mwisimaeli.

18Kalebu mwana wa Hesironi, kutoka kwa bibi zake wawili Azuba na Yerioti, alizaa: Yeseri, Sobabu na Ardoni.

19Azuba alipokufa, Kalebu akaoa Efurata aliyemuzalia Huri.

20Huri alikuwa baba ya Uri, naye Uri alizaa Besaleli.

21Hesironi alipokuwa na umri wa miaka makumi sita, akaoa binti ya Makiri, dada ya Gileadi. Huyu akamuzalia mwana jina lake Segubu.

22Segubu alizaa Yairi ambaye alitawala miji mikubwa makumi mbili na mitatu katika inchi ya Gileadi.

23Lakini falme za Gesuri na Aramu ziliwashambulia na kuwanyanganya miji ya Yairi, Kenati pamoja na vijiji vyake, jumla ya miji ilikuwa makumi sita. Hao wote walikuwa wazao wa Makiri, baba ya Gileadi.

24Nyuma ya kufa kwa Hesironi, Kalebu akaoa Efurata, mujane wa baba yake Hesironi. Efurata akamuzalia Kalebu mwana jina lake Asuri, aliyekuwa mwanzilishi wa muji wa Tekoa.

25Yerameli, muzaliwa wa kwanza wa Hesironi, alikuwa na wana watano: Ramu, muzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya.

26Yerameli alikuwa na muke mwingine jina lake Atara. Yeye akamuzalia Yerameli mwana, jina lake Onamu.

27Wana wa Ramu, muzaliwa wa kwanza wa Yerameli, walikuwa: Masi, Yamini na Ekeri.

28Wana wa Onamu walikuwa: Samayi na Yada. Nao wana wa Samayi walikuwa Nadabu na Abisuri.

29Abisuri akaoa muke, jina lake Abihaili, naye akamuzalia wana wawili: Abani na Molidi.

30Wana wa Nadabu walikuwa: Seledi na Apaimu. Seledi akakufa bila watoto.

31Mwana wa Apaimu alikuwa: Isi.

Mwana wa Isi: Sesani.

Mwana wa Sesani: Alai.

32Wana wa wawili wa Yada, ndugu ya Samai: Yeteri na Yonatani.

Yeteri alikufa bila watoto.

33Yonatani alikuwa na wana wawili: Peleti na Zaza. Wote hawa ni wazao wa Yerameli.

34Sesani hakukuwa na watoto wa kiume; alikuwa na wabinti tu. Hata hivyo, alikuwa na mutumwa wa Mumisri, jina lake Yara.

35Hivyo, Sesani akamupa Yara mutumwa wake, mumoja kati ya wabinti zake kuwa muke wake, naye akamuzalia mwana jina lake Atai.

36-41Atai alizaa Natani,

Natani alizaa Zabadi,

Zabadi alizaa Efulali,

Efulali alizaa Obedi,

Obedi alizaa Yehu,

Yehu alizaa Azaria,

Azaria alizaa Helesi,

Helesi alizaa Elasa,

Elasa alizaa Sisamai,

Sisamai alizaa Salumu,

Salumu alizaa Yekamia,

Yekamia alizaa Elisama.

42Muzaliwa wa kwanza wa Kalebu, ndugu ya Yerameli, aliitwa Mesa. Mesa alikuwa baba ya: Zifu, Zifu baba ya Maresa, Maresa alizaa Hebroni.

43Wana wa Hebroni walikuwa: Kora, Tapua, Rekemu na Sema.

44Sema alizaa Rahamu na babu ya Rekemu.

Rekemu alizaa Samai.

45Samai alizaa Maoni,

Maoni alizaa Beti-Suri.

46Kalebu alikuwa na habara, jina lake Efa. Huyu akamuzalia wana wengine watatu: Harani, Moza na Gazezi. Harani alizaa Gazezi.

47Yadai alikuwa na wana sita: Regemu, Yotamu, Gesani, Peleti, Efa na Safu.

48-49Kalebu alikuwa na habara mwingine jina lake Maka. Huyu akamuzalia wana hawa: Seberi, Tirana, Safu aliyekuwa mwanzilishi wa muji wa Madimana, na Sewa aliyekuwa mwanzilishi wa muji wa Makibena na Gibea. Kalebu alikuwa vilevile na binti, jina lake Akisa.

50Kalebu alikuwa na wazao wengine vilevile toka kwa muke wake Efurata.

Wana wa Huri, muzaliwa wake wa kwanza, walikuwa: Sobali, mwanzilishi wa muji wa Kiriati-Yearimu;

51Salma, mwanzilishi wa muji wa Betelehemu, na Harefu, mwanzilishi wa muji wa Beti-Gaderi.

52Sobali, mwanzilishi wa muji wa Kiriati-Yearimu, alikuwa vilevile babu ya: watu wa Haroe, na nusu ya wakaji wa muji wa Menuhoti,

53pamoja na ukoo hizi zilizoishi Kiriati-Yearimu: Waitiri, Waputi, Wasumati na Wamisira. (Wazorati na Waestaoli walitoka katika watu wale).

54Salma, mwanzilishi wa muji wa Betelehemu alikuwa babu ya: Wanetofati, Waataroti-Beti-Yoabu na nusu ya Wamenahati ni kusema Wazori.

55Watu wa jamaa hizi waliishi katika muji wa Yabesi: Watirati, Wasimeati na Wasukati. Wao ndio Wakeni waliotoka katika uzao wa Hamati, aliyekuwa babu ya waliokuwa wa ukoo wa Warekabu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help