Nehemia UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIKitabu hiki ni mufululizo wa kitabu kilichotangulia, ni kusema Ezra. Nehemia aliishi wakati wa Ezra na alikuwa musimamizi mukubwa katika utawala wa Artasasta, mufalme wa Persia. Yeye alipata ruhusa kutoka kwa mukubwa wake arudi Yerusalema ajishugulishe na kutengeneza maisha ya siasa, uchumi na jamii (sura 1.1–2.10). Mara tu alipofika kule, ingawa alikutana na upinzani kutoka kwa waadui wamoja, aliungwa mukono na wamoja kati ya wanainchi wenzake wakajenga kuta za Yerusalema (sura 2.11–7.72). Nehemia na Ezra walikuwa pale wakati wa mukutano mukubwa wa kidini ambamo Ezra alihutubia juu ya sheria ya Mungu.Watu walirudilia tena maagano yao kwa Mungu (sura 8.1–10.40). Nyuma ya kutoa mipango mbalimbali iliyoelekea hasa mambo ya siasa, Nehemia akasimamia muzinduo wa kuta zilizojengwa upya (11.1–12.43), kisha akaendelea na mambo mengine ya matengenezo ya dini (sura 12.44–13.31).