1 Mambo ya Siku 20 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Daudi ananyanganya muji wa Raba(2 Sam 12.26-31)

1Ilipokuwa wakati wa kipwa, wakati ambapo wafalme wanaenda kwa vita, Yoabu akaongoza jeshi na kuharibu inchi ya Waamoni, akaenda vilevile na kuzunguka muji wa Raba kwa vita. Lakini Daudi alibaki kule Yerusalema. Naye Yoabu akashambulia muji wa Raba na kuuteka. hivyo Wafilistini wakashindwa.

5Kukatokea tena vita na Wafilistini. Naye Elihanani mwana wa Yairi akamwua Lami ndugu ya Goliati wa muji wa Gati ambaye mupini wa mukuki wake ulikuwa kama muti wa mufumaji wa nguo.

6Nyuma kukatokea tena vita kule Gati ambako kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa murefu sana, na vidole sita katika kila mukono, na vidole sita katika kila muguu, kwa jumla vidole makumi mbili na vine. Yeye vilevile alikuwa wa uzao wa majitu.

7Naye alipowatukana Waisraeli, Yonatani mwana wa Simea, ndugu ya Daudi, akamwua.

8Hao walikuwa wazao wa majitu kule Gati, nao wakauawa na Daudi pamoja na watumishi wake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help