1Yawe anatawala!
Furahi, ee dunia!
Mufurahi, enyi visanga vingi!
2Mawingu na giza nzito vinamuzunguka;
haki na sheria ni musingi wa utawala wake.
3Moto unatangulia mbele yake,
na kuwateketeza waadui zake pande zote.
4Umeme wake unaangaza ulimwengu;
dunia inauona na kutetemeka.
5Milima inayeyuka kama inta mbele ya Yawe,
mbele ya Bwana wa dunia yote.
6Mbingu zinatangaza haki yake;
na mataifa yote yanauona utukufu wake.
7Wote wanaoabudu sanamu
na kujisifia miungu ya bure
wanafezeheshwa.
Miungu yote inainama mbele yake.
8Watu wa Sayuni wanasikia hayo na kufurahi;
watu wa Yuda wanashangilia
kwa ajili ya hukumu zako, ee Mungu.
9Wewe Yawe ni mukubwa juu ya dunia yote;
wewe unatukuzwa juu ya miungu yote.
10Yawe anawapenda wale wanaochukia uovu,
anayalinda maisha ya watu wake,
anawaokoa kutoka makucha ya waovu.
11Mwangaza unamwangazia mutu wa haki,
nayo furaha ni kwa watu wenye moyo wa usawa.
12Mufurahi kwa sababu ya Yawe, enyi watu wa haki;
mumushukuru kwa ajili ya utakatifu wake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.