1Yawe akamwambia Musa: Uwaambie makuhani, wana wa Haruni, kwamba kusikuwe mutu yeyote kati yao atakayejichafua kwa kugusa maiti ya watu wa jamaa yake,
2isipokuwa kama ni maiti ya ndugu yake wa karibu, ni kusema mama yake, baba yake, mwana wake, binti yake, ndugu yake
3au dada yake ambaye (aliyekuwa wa jamaa yake ya karibu), naye hajaolewa bado.
4Yeye, akiwa mwenye madaraka katika jamaa yake, asijichafue.
5Wazao wa Haruni wasijinyoe upaa kwa kuomboleza wala wasikate pembe za ndevu zao wala kujichanja chanjo juu ya mwili. Ang. Law 19.27-28; Kumb 14.1
6Watakuwa watakatifu kwa Mungu wao wala wasichafue jina la Mungu wao. Maana wao ndio wanaotolea zile sadaka Yawe anazopewa kwa moto, ni kusema chakula cha Mungu. Basi, wanapaswa kuwa watakatifu.
7Kwa sababu kuhani ametakaswa kwa ajili ya Mungu wake, asioe kahaba wala mwanamuke asiyekuwa bikira wala aliyefukuzwa na mume wake.
8Utamutambua kuhani kuwa aliyetakaswa, maana yeye ndiye anayetolea sadaka ya mukate wa Mungu wako. Utamutambua kuwa mutakatifu, maana mimi Yawe ninayekutakasa wewe ni mutakatifu.
9Binti wa kuhani yeyote akijichafua kwa kufanya ukahaba, atateketezwa kwa moto maana anamuchafua baba yake.
10Kuhani Mukubwa ni mukubwa kati ya wandugu zake, naye amemiminiwa mafuta ya kupakaa juu ya kichwa chake, na kutakaswa kusudi avae nguo takatifu. Asiache nywele zake kuwa ovyo wala asipasue nguo zake kwa kuomboleza.
11Asikaribie maiti wala kujichafua kwa maiti hata kama ni ya baba yake au ya mama yake.
12Kwa sababu ametakaswa kwa kupakwa mafuta ya Mungu wake juu ya kichwa, basi asiondoke katika Pahali Patakatifu wala asipachafue. Mimi ni Yawe.
13Kuhani Mukubwa anaweza tu kumwoa binti ambaye ni bikira.
14Haruhusiwi kuoa mwanamuke mujane, mwanamuke asiyekuwa bikira, wala kahaba. Anapaswa kuoa bikira kutoka watu wake mwenyewe
15kusudi asichafue watoto wake mwenyewe. Mimi ni Yawe niliyemutakasa.
16Yawe akamwambia Musa:
17Umwambie Haruni hivi: Muzao wako yeyote katika vizazi vyote vinavyokuja ambaye ana kilema juu ya mwili, haruhusiwi kukaribia na kunitolea mimi Mungu wake sadaka ya mukate.
18Mutu yeyote anayekuwa na kilema, kipofu, aliyelemaa, mwenye uso uliokatwakatwa, mwenye kiungo kirefu kuliko kawaida,
19mwenye muguu au mukono uliovunjika,
20mwenye kigongo, mutu mufupi kuliko kawaida, asiyeona sawasawa, mwenye kivimba, mwenye upele au mutu anayekuwa towashi, asikaribie kumutolea Mungu mukate wake.
21Muzao yeyote wa kuhani Haruni mwenye kilema asikaribie kwa kunitolea sadaka za kuteketezwa kwa moto. Kwa vile ana kilema, basi, asikaribie kunitolea mimi Mungu mukate wangu.
22Mutu huyo anaweza kula mukate wa Mungu wake, vitu vitakatifu na vile vitakatifu kabisa.
23Lakini asilikaribie lile pazia wala ile mazabahu maana ana kilema, asipate kuchafua Pahali Patakatifu, kwa sababu mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.
24Musa akamwelezea Haruni na wana wake na Waisraeli wote mambo hayo yote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.