Zaburi 120 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kuomba musaadaKushika sheria ya Mungu

1Wimbo wa safari za kidini.

Katika taabu yangu nilimwita Yawe,

naye akanijibu.

2Uniokoe, ee Yawe,

kutoka watu wadanganyifu na waongo.

3Enyi watu wadanganyifu, mutapewa kitu gani?

Mutaazibiwa namna gani?

4Kwa mishale mikali ya waaskari,

kwa makaa ya moto mukali!

5Ole wangu maana ninaishi kama mugeni huko Meseki;

ninaishi kama mugeni katika mahema ya Kedari.

6Nimeishi muda murefu sana

kati ya watu wanaochukia amani!

7Ninaposema kwamba ninataka amani,

wao wanataka tu vita.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help