1Wimbo wa safari za kidini.
Katika taabu yangu nilimwita Yawe,
naye akanijibu.
2Uniokoe, ee Yawe,
kutoka watu wadanganyifu na waongo.
3Enyi watu wadanganyifu, mutapewa kitu gani?
Mutaazibiwa namna gani?
4Kwa mishale mikali ya waaskari,
kwa makaa ya moto mukali!
5Ole wangu maana ninaishi kama mugeni huko Meseki;
ninaishi kama mugeni katika mahema ya Kedari.
6Nimeishi muda murefu sana
kati ya watu wanaochukia amani!
7Ninaposema kwamba ninataka amani,
wao wanataka tu vita.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.