1Rakeli alipoona kwamba hajamuzalia Yakobo watoto, alimwonea Lea dada yake wivu, akamwambia Yakobo: “Unipatie watoto, kama sivyo, nitakufa.”
2Yakobo akamukasirikia Rakeli na kumwambia: “Mimi nimekuwa pahali pa Mungu aliyekuzuia kupata watoto?”
3Rakeli akamujibu: “Mujakazi wangu Biliha yuko. Lala naye kusudi azae watoto pahali pangu, nami vilevile nipate watoto kutokana naye.”
4Kwa hiyo Rakeli akamupa Yakobo mujakazi wake, Biliha akuwe muke wake, naye akalala naye.
5Biliha akapata mimba na kumuzalia Yakobo mutoto mwanaume.
6Rakeli akasema: “Mungu amenitendea sawa, amesikia kilio changu na kunipa mutoto mwanaume.” Akamwita mutoto yule Dani.
7Biliha, mujakazi wa Rakeli, akapata mimba tena na kumuzalia Yakobo mutoto wa pili mwanaume.
8Halafu Rakeli akasema: “Nimepigana mapigano makubwa na dada yangu, nami nimeshinda.” Kwa hiyo akamwita mutoto yule Nafutali.
9Lea alipoona ameacha kuzaa, alimutwaa Zilpa, mujakazi wake, na kumupa Yakobo kusudi akuwe muke wake.
10Zilpa akamuzalia Yakobo mutoto mwanaume.
11Lea akasema: “Bahati njema.” Kwa hiyo akamwita mutoto yule Gadi.
12Zilpa, mujakazi wa Lea, akamuzalia Yakobo mutoto wa pili mwanaume.
13Lea akasema: “Bahati njema! Sasa wanawake wataniita heri.” Kwa hiyo akamwita mutoto yule Aseri.
14Ikakuwa wakati wa mavuno ya ngano, Rubeni alikwenda kwenye shamba na kule akapata matunda ya dudai, akamuletea mama yake Lea. Rakeli akamwambia Lea: “Tafazali, unipe sehemu ya dudai za mwana wako.”
15Lakini Lea akamwambia kwa ukali: “Unazani ni jambo dogo kuninyanganya mume wangu na sasa unataka kutwaa dudai za mwana wangu?”
Rakeli akamujibu: “Ikiwa utanipa dudai za mwana wako, Yakobo atalala kwako leo.”
16Basi, magaribi Yakobo alipokuwa anarudi toka kwenye shamba, Lea alitoka kwenda kumupokea, akamwambia: “Leo unapaswa kulala nami, maana nimekununua kwa dudai za mwana wangu.” Hivyo Yakobo akalala kwa Lea usiku ule.
17Mungu akasikiliza ombi la Lea, naye akapata mimba na kumuzalia Yakobo mutoto wa tano mwanaume.
18Lea akasema: “Mungu amenipa mushahara wangu kwa sababu nilimupa mume wangu mujakazi wangu.” Kwa hiyo akamwita mutoto yule Isakari.
19Lea akapata mimba tena na kumuzalia Yakobo mutoto wa sita mwanaume.
20Akasema: “Mungu amenipa zawadi bora. Sasa mume wangu ataniheshimu kwa maana nimemuzalia watoto sita wanaume.” Kwa hiyo akamwita mutoto yule Zabuluni.
21Kisha akazaa mutoto mwanamuke, akamwita Dina.
22Kisha Mungu akamukumbuka Rakeli, akakubali ombi lake na kumujalia kupata watoto.
23Rakeli akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume, akasema: “Mungu ameniondolea haya yangu.”
24Kwa hiyo akamwita mutoto yule Yosefu akisema: “Yawe aniongezee mutoto mwingine mwanaume.”
Yakobo anatajirika25Nyuma Rakeli kuzaa Yosefu, Yakobo akamwambia Labani: “Uniruhusu nirudie kwetu, katika inchi yangu.
26Unipe wake zangu na watoto wangu ambao nimejipatia kutokana na utumishi wangu kwako, niondoke nao. Unajua kwamba nimekutumikia vema.”
27Lakini Labani akamwambia: “Basi uniruhusu nami niseme. Nimetambua kwa kuaguza kwamba Yawe amenibariki kwa sababu yako.
28Sema mushahara wako, nami nitakulipa.”
29Yakobo akamwambia: “Wewe mwenyewe unajua jinsi nilivyokutumikia, na jinsi nilivyowatunza nyama wako.
30Mbele sijakuja ulikuwa na mali chache tu lakini tangu nifike, mali yako imeongezeka kwa wingi sana, na Yawe amekubariki kila fasi nilikokwenda. Lakini sasa, nitatunza wakati gani jamaa yangu mwenyewe?”
31Labani akamwuliza: “Nikupatie nini?”
Yakobo akamujibu: “Hautanipatia kitu chochote. Nitaendelea kuwatunza nyama wako ikiwa utanifanyia jambo hili:
32Uniruhusu nipite kati ya nyama wako wote leo, nitenge katika kundi kila nyama mwenye madoadoa na matakamataka, kila nyama mweusi, kati ya kondoo na mbuzi wanaokuwa na madoadoa na matakamataka. Huo ndio utakaokuwa mushahara wangu.
33Hivyo, siku zinazokuja, uaminifu wangu utaonekana waziwazi utakapokuja kuangalia mushahara wangu. Mbuzi yeyote asiyekuwa na madoadoa au matakamataka, au kondoo yeyote asiyekuwa mweusi akionekana katika kundi langu, yule atakuwa ameibiwa.”
34Labani akasema: “Sawa! Ikuwe kama vile ulivyosema.”
35Lakini siku hiyohiyo Labani akakwenda akatenga beberu wote wenye mistari na madoadoa, mbuzi wote dike waliokuwa na madoadoa na matakamataka, kila nyama aliyekuwa na weupe kwenye mwili wake, na kila kondoo mweusi, akawaweka chini ya ulinzi wa wana wake.
36Labani akajitenga na Yakobo umbali wa mwendo wa siku tatu, naye Yakobo akabaki akichunga nyama wa Labani waliobaki.
37Basi, Yakobo akatwaa fito mbichi za miti ya mulubna, lozi na mwaramoni, akazimenya maganda mistari nyeupe ionekane katika fito hizo.
38Akasimamisha fito zile alizomenya maganda mbele ya nyama katika mabirika ya kukunyweshea maji, pahali ambapo nyama walikuja kukunywa maji. Na kwa sababu nyama walipata mimba walipokuja kunywa maji,
39wakapata mimba mbele ya zile fito; wakazaa nyama wenye mistari, matakamataka na madoadoa.
40Yakobo akatenga hao wana-kondoo, kisha akawaelekeza kwenye nyama wenye mistari na weusi katika kundi la Labani. Kwa njia hii, Yakobo akajipatia kundi lake mwenyewe, wala hakulichanganya na lile la Labani.
41Ikakuwa kila mara ulipofika wakati wa nyama wenye afya kupata mimba, Yakobo aliweka zile fito mbele yao katika mabirika ya kukunyweshea maji, kusudi wapate mimba kwenye fito zile.
42Lakini hakuweka fito zile mbele ya nyama zaifu walipopata mimba. Hivi, nyama zaifu wakakuwa wa Labani, na wenye afya wakakuwa wa Yakobo.
43Basi, Yakobo akatajirika sana, akakuwa na makundi makubwa ya nyama, wajakazi na watumwa, ngamia na punda.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.