1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2Wewe mwanadamu, geukia upande wa kusini, uhubiri juu ya inchi ya kusini, juu ya wakaaji wa pori la Negebu.
3Uwaambie wasikilize neno la Yawe. Uwaambie kwamba Bwana wao Yawe anasema hivi: Nitawasha moto kwako, nao utateketeza miti yote, mibichi na yenye kukauka; utaenea tangu kusini mpaka kaskazini wala hakuna atakayeweza kuzimisha ndimi zake. Nao utaunguza watu wote.
4Watu wote watajua kwamba ni mimi Yawe niliyeuwasha na hautazimika.
5Kisha nami nikasema: Ee Bwana wetu Yawe! Watu wanalalamika juu yangu na kusema: Huyu akisema, ni mafumbo tu!
Upanga wa Yawe6Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
7Wewe mwanadamu, ugeukie upande wa Yerusalema, uhubiri juu ya nafasi zake za kutambikia, na kutoa unabii juu ya inchi ya Waisraeli.
8Uwaambie Waisraeli kwamba:
Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe ninakuja kupambana nanyi. Nitauchomoa upanga wangu ndani ya mufuko wake na kuwaua watu wema na wabaya.
9Tangia kaskazini mpaka kusini, nitawaua watu wote, wema na wabaya, kwa upanga wangu.
10Watu wote watajua kwamba mimi Yawe ndiye niliyeuchomoa upanga ndani ya mufuko wake na wala hautarudishwa tena ndani.
11Nawe mwanadamu, ujikunje kama mutu aliyekata tamaa, uomboleze mbele yao.
12Wakikuuliza hivi: Kwa nini unaomboleza? Utawaambia: Ninaomboleza kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila mutu atavunjika moyo, mikono yao yote itaregea; kila mutu anayeishi atazimia na magoti yao yataregea. Habari hizo zinakuja kweli, nazo zinatimia. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.
13Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
14Wewe mwanadamu, toa unabii useme:
Yawe anasema hivi:
Upanga! Kweli, upanga umenolewa,
nao umeangarishwa vilevile.
15Umenolewa kusudi ufanye mauaji,
umeangarishwa umetemete kama umeme!
16Umenolewa na kuangarishwa
uwekwe katika mukono wa mwuaji.
17Wewe mwanadamu, ulie na kuomboleza
upanga huo umenyooshwa juu ya watu wangu,
juu ya wakubwa wote wa Waisraeli.
Wataangamizwa kwa upanga pamoja na watu wangu.
Ujipigepige kifua kwa huzuni.
18Hilo litakuwa jaribu gumu sana.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
19Wewe mwanadamu, utabiri!
Piga mikono,
upanga ufanye kazi yake,
mara mbili, mara tatu.
Huo ni upanga wa mauaji
nao unawazunguka.
20Kwa hiyo wamevunjika moyo
na wengi wanaanguka.
Nimeiweka chongo ya upanga katika milango yao yote.
Umefanywa uangae kama umeme,
umengarishwa kwa ajili ya mauaji.
21Ewe upanga, shambulia upande wa kuume,
shambulia upande wa kushoto;
elekeza chongo yako pande zote.
22Nami nitapiga mikono,
kasirani yangu itatosheka.
Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.
Uamuzi wa Yerusalema23Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
24Wewe mwanadamu! Chora njia mbili ambapo upanga wa mufalme wa Babeli utapitia. Njia zote mbili zianzie katika inchi moja. Kwa mwanzo wa kila njia utaweka kitambulisho cha kuonyesha upande muji unapokuwa.
25Utachora njia upanga utakapopitia kwenda kuufikilia muji Raba wa Waamoni, na njia ingine inayoelekea Yerusalema wenye kuzungukwa na kuta katika inchi ya Yuda.
26Mufalme wa Babeli anasimama kwa mwanzo wa hizo njia mbili, kwenye masanganjia, apate kuaguza. Anatikisa mishale, anauliza shauri la sanamu ya miungu yake na kuchunguza maini ya nyama.
27Mushale ulioangukia kwa upande wa mukono wake wa kuume, ulionyesha Yerusalema. Pale wataweka vifaa vya vita kwa kuubomoa. Anaamuru mauaji, kelele za vita zipigwe, vifaa vya vita kwa kubomoa milango viwekwe, lundo ya udongo na minara kwa kuushambulia muji viwekwe vilevile.
28Lakini watu wa Yerusalema watauzania kuwa ni utabiri wa uongo kwa sababu ya mapatano waliyofanya. Hata hivyo unabii huu utawakumbusha uovu wao na kusababisha kukamatwa kwao.
29Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wote wataweza kuziona zambi zenu. Kila mutu atajua jinsi munavyokuwa na makosa. Kila kitendo munachotenda kinaonyesha zambi zenu. Ninyi mutapata azabu nami nitawatia katika mikono ya waadui zenu.
30Nawe, mufalme wa Waisraeli, wewe ni mupotovu kabisa. Siku yako imefika, siku ya azabu yako ya mwisho.
31Bwana wetu Yawe anasema hivi: tosha kitambulisho chako cha kifalme na taji yako, maana mambo hayatabaki kama yalivyokuwa. Wanaokuwa chini watanyanyuliwa, wanaokuwa juu watashushwa!
32Uharibifu! Uharibifu! Hakuna chochote katika muji huu nitakachoacha. Lakini mbele ya hayo kutafika kwanza yule ambaye nimemupa mamlaka ya kuuazibu, ambaye mimi nitamupa muji ule.
Azabu ya Waamoni33Ewe mwanadamu, tabiri juu ya Waamoni na maneno yao ya kuwachekelea Waisraeli: Uwaambie kwamba ninasema hivi:
Upanga, upanga!
Upanga umenyooshwa kwa kuua,
umenolewa upate kuangamiza,
umengarishwa uangae kama umeme.
34Wakati ninyi mumetulia katika maono yenu madanganyifu na utabiri wenu wa uongo, upanga utakuwa tayari kukata shingo za waasi na waovu. Siku imetimia ambapo maovu yenu yataazibiwa.
35Sasa rudisha upanga ndani ya mufuko wake! Nitawahukumu pahali palepale mulipoumbwa, katika inchi mulipozaliwa.
36Nitawamwangia kasirani yangu. Moto wa kasirani yangu nitaupuliza juu yenu. Nitawatoa katika mikono ya watu waovu, watu hodari wa kuangamiza.
37Mutakuwa kama kuni ndani ya moto, damu yenu itamwangika katika inchi. Mutu hatawakumbuka tena. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.