1Kama mutu anatoa sadaka ya amani na sadaka yake ni ngombe dume au dike, nyama huyo asikuwe na kilema mbele yangu.
2Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja kwenye mulango wa hema la mukutano. Hao makuhani wazao wa Haruni watainyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.
3Mafuta yote yanayofunika na yanayokuwa juu ya matumbotumbo ya nyama wa sadaka hiyo ya amani atayateketeza kama sadaka Yawe anayotolewa kwa moto.
4Atatoa vilevile zile figo mbili na mafuta yake pamoja na ile sehemu bora ya maini.
5Wazao wa Haruni wataiteketeza juu ya mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa inayokuwa juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.
6Kama sadaka hiyo ya amani unayomutolea Yawe ni kutoka kundi la kondoo au mbuzi, basi achaguliwe dume au dike asiyekuwa na kilema.
7Kama mutu atatoa mwana-kondoo kuwa sadaka yake, basi atamutolea mbele ya Yawe,
8akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Makuhani wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.
9Kisha, kutoka katika sadaka hiyo ya amani Yawe anayotolewa kwa moto, atamutolea sehemu hizi: mafuta yake, mukia muzima wenye mafuta uliokatwa karibu kabisa na uti wa mugongo pamoja na mafuta yote yanayofunika matumbotumbo na mafuta yote yanayokuwa kwenye matumbotumbo,
10zile figo mbili na mafuta yake pamoja na sehemu bora ya maini.
11Kuhani ataviteketeza hivyo vyote juu ya mazabahu kama vile chakula Yawe anachotolewa kwa moto.
12Kama sadaka yake ni mbuzi, basi atamutolea mbele ya Yawe
13akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.
14Kisha, atamutolea Yawe mafuta yote yanayofunika matumbotumbo
15na zile figo mbili na mafuta yake pamoja na sehemu bora ya maini.
16Kuhani ataviteketeza juu ya mazabahu kama chakula kinachotolewa kwa Yawe kwa moto kutoa harufu ya kumupendeza Mungu. Mafuta yote ni ya Yawe.
17Ndiyo maana munapaswa kufuata sharti hili siku zote na pahali popote mutakapokaa. Musikule hata kidogo mafuta wala damu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.