Kutoka 12 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Pasaka(Kumb 16.1-8)

1Yawe akamwambia Musa na Haruni, walipokuwa wangali katika inchi ya Misri: Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu

15Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.

16Siku ya kwanza na siku ya saba mutakuwa na mukutano mutakatifu. Katika siku hizo mbili hamutaruhusiwa kufanya kazi yoyote isipokuwa kazi ya lazima ya kutayarisha chakula.

17Mutashika sikukuu hii ya Mikate Isiyotiwa Chachu kama ukumbusho wa siku nilipowatoa ninyi vikundi vya Israeli kutoka Misri. Sikukuu hiyo itashikwa na vizazi vyenu vyote vinavyokuja, kama agizo la milele.

18Basi, mutakula mikate isiyotiwa chachu kuanzia magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, mpaka magaribi ya siku ya makumi mbili na moja ya mwezi uleule wa kwanza.

19Katika siku hizo saba, musikuwe na chachu yoyote katika nyumba zenu. Mutu yeyote, akuwe mugeni au mwenyeji, akikula kitu kilichotiwa chachu, ataondolewa katika kusanyiko la Waisraeli.

20Popote pale munapoishi, hamutakula chochote kilichotiwa chachu. Munapaswa kula mikate isiyotiwa chachu.”

Pasaka ya kwanza

21Basi, Musa akawaita wazee wote wa Waisraeli, akawaambia: “Muchague kila mumoja wenu, kulingana na jamaa yake, mwana-kondoo na kumuchinja kwa sikukuu ya Pasaka.

22Mutatwaa majani ya hisopo na kuyachovya katika damu ndani ya beseni na kupakaa vizingiti na miimo yote miwili ya milango ya nyumba zenu. Mutu yeyote asitoke inje ya nyumba usiku ule mpaka asubui.

23Maana Yawe atapita kuwaua Wamisri. Lakini atakapoona damu iliyopakwa kwenye vizingiti na miimo ya nyumba zenu, atapita na wala hatamuruhusu mwangamizaji kuingia katika nyumba zenu na kuwaua. Ang. Ebr 11.28

24Mushike jambo hili ninyi na wazao wenu kama agizo la milele.

25Mutakapoingia katika inchi ile ambayo Yawe atawapa, kama alivyoahidi, munapaswa kulitimiza.

26Kila wakati watoto wenu watakapowauliza: ‘Jambo hili lina maana gani?’,

27ninyi mutawajibu: ‘Hii ni sadaka ya Pasaka kwa Yawe, kwa sababu alipita nyumba za Waisraeli katika inchi ya Misri. Aliwaua Wamisri, lakini sisi hakutuua.’ ”

Waisraeli wakainamisha vichwa na kumwabudu Yawe.

28Kisha Waisraeli wakaenda, wakafanya kama vile walivyoambiwa na Musa na Haruni kulingana na amri ya Yawe.

Pigo la kumi: Kuuawa kwa wazaliwa wa kwanza wa Wamisri

29Katikati ya usiku, Yawe akawaua wazaliwa wa kwanza wote wa Misri. Wote walikufa, tangu muzaliwa wa kwanza wa mufalme wa Misri, murizi wa ufalme, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mufungwa katika kifungo. Hata wazaliwa wa kwanza wa nyama nao walikufa. Ang. Kut 4.22-32

30Basi mufalme, watumishi wake na wakaaji wote wa Misri wakaamuka usiku. Kukakuwa kilio kikubwa katika inchi yote ya Misri kwa maana hakukuwa hata nyumba moja ambamo mutu hakukufa.

31Halafu mufalme wa Misri akaita Musa na Haruni, usiku uleule, akawaambia: “Musimame! Muondoke kati ya watu wangu. Muende, ninyi pamoja na wale Waisraeli, mumutumikie Yawe kama vile mulivyosema.

32Mutwae makundi yenu ya kondoo na ngombe, muondoke. Muniombee na mimi baraka.”

33Wamisri wakawasukuma Waisraeli waondoke haraka, wakisema: “Hakika tutakufa sisi wote!”

34Basi, Waisraeli wakatwaa unga wao uliopondwa mbele haujatiwa chachu na mabakuli yao ya kupondea mikate walikuwa wamezifunga kwa nguo na kubeba juu ya mabega.

35Waisraeli walikuwa wamekwisha kufanya kama vile Musa alivyowaagiza pale mbele. Waliwaomba Wamisri wawapatie vyombo vya feza na zahabu na nguo. Ang. Kut 3.21-22

36Naye Yawe alikwisha kuwafanya Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Wamisri, nao Wamisri wakawapa kila kitu walichoomba. Ndivyo Waisraeli walivyonyanganya Wamisri mali yao.

Waisraeli wanaondoka Misri

37Waisraeli waliondoka katika muji wa Ramesesi, wakasafiri kwa miguu kuelekea Sukoti. Walikuwa wanaume yapata elfu mia sita, bila kuhesabu wanawake na watoto.

38Kulikuwa vilevile kundi la watu wengine waliokwenda pamoja nao na mifugo mingi, kondoo na ngombe.

39Kwa sababu walikuwa wameondoka Misri kwa haraka, hawakuweza kutayarisha chakula cha safari, ila tu ule unga uliopondwa bila kutiwa chachu. Basi, wakapika mikate isiyotiwa chachu.

40Waisraeli walikuwa wameishi katika inchi ya Misri kwa muda wa miaka mia ine na makumi tatu. Ang. Mwa 15.13; Gal 3.17

41Katika siku ya mwisho ya mwaka wa mia ine na makumi tatu, siku ileile ndipo makabila yote ya Yawe yaliondoka katika inchi ya Misri.

42Usiku ule ambao Yawe alikesha kwa kuwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri, unapaswa kukumbukwa na Waisraeli wote na vizazi vyao vyote, kama usiku wa kukesha kwa heshima ya Yawe.

Utaratibu wa Pasaka

43Yawe akamwambia Musa na Haruni: “Haya ndiyo maagizo juu ya Pasaka. Mugeni yeyote hatashiriki chakula cha Pasaka.

44Lakini mutumwa yeyote aliyenunuliwa kwa feza, nyuma ya kumutahiri, ataruhusiwa kushiriki.

45Musafiri yeyote, wala mutumishi yeyote wa mushahara, hatashiriki chakula hicho.

46Mwana-kondoo wa Pasaka atakuliwa katika nyumba moja. Hamutatoa nyama yoyote inje ya nyumba alimochinjiwa, wala hamutavunja hata mufupa mumoja wa nyama wa Pasaka. Ang. Hes 9.12; Yn 19.36

47Waisraeli wote pamoja watashika sikukuu hiyo.

48Mugeni yeyote anayeishi kati yenu akipenda kushiriki sikukuu ya Pasaka, anapaswa kwanza kutahiri wanaume wote wa nyumba yake. Halafu atahesabiwa kuwa kama mwenyeji na kuruhusiwa kushiriki. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa asishiriki hata kidogo.

49Sheria zilezile zitaelekea Mwisraeli aliyezaliwa katika inchi na wageni watakaoishi kati yenu.”

50Waisraeli wote walitii sheria hiyo na kufanya kama vile Yawe alivyowaagiza Musa na Haruni.

51Siku hiyohiyo Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri kwa makundi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help