Zaburi 75 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu ni mwamuzi wa haki

1Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu”. Zaburi ya Asafu: wimbo.

2Tunakushukuru, ee Mungu,

tunakushukuru!

Tunatangaza ukubwa wa jina lako

na kueleza matendo yako makubwa.

3Mungu anasema: “Mimi nimeweka wakati kamili!

Wakati huo nitahukumu kwa haki.

4Inchi ikitetemeka na vyote vinavyokuwa ndani yake,

mimi ndiye ninayeimarisha misingi yake.

5Ninawaambia wenye kiburi:

‘Mwache kiburi’,

na waovu: ‘Musiote mapembe!

6Musijione kuwa watu wa maana sana,

wala kusema maneno ya majivuno.’ ”

7Ukubwa hautoki mashariki au magaribi,

wala hautoki katika jangwa au kwa milima.

8Mungu mwenyewe ndiye mwamuzi;

anamushusha mumoja na kumwinua mwingine.

9Yawe anashika kikombe katika mukono,

kimejaa divai kali ya hasira yake.

Anaimimia, nao waovu wote wanaikunywa;

wanaikunywa mpaka tone la mwisho.

10Lakini mimi nitafurahi milele,

nitamwimbia Mungu wa Yakobo sifa.

11Atavunja mapembe yote ya watu waovu;

lakini ataotesha mapembe ya watu wa haki.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help