1Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu”. Zaburi ya Asafu: wimbo.
2Tunakushukuru, ee Mungu,
tunakushukuru!
Tunatangaza ukubwa wa jina lako
na kueleza matendo yako makubwa.
3Mungu anasema: “Mimi nimeweka wakati kamili!
Wakati huo nitahukumu kwa haki.
4Inchi ikitetemeka na vyote vinavyokuwa ndani yake,
mimi ndiye ninayeimarisha misingi yake.
5Ninawaambia wenye kiburi:
‘Mwache kiburi’,
na waovu: ‘Musiote mapembe!
6Musijione kuwa watu wa maana sana,
wala kusema maneno ya majivuno.’ ”
7Ukubwa hautoki mashariki au magaribi,
wala hautoki katika jangwa au kwa milima.
8Mungu mwenyewe ndiye mwamuzi;
anamushusha mumoja na kumwinua mwingine.
9Yawe anashika kikombe katika mukono,
kimejaa divai kali ya hasira yake.
Anaimimia, nao waovu wote wanaikunywa;
wanaikunywa mpaka tone la mwisho.
10Lakini mimi nitafurahi milele,
nitamwimbia Mungu wa Yakobo sifa.
11Atavunja mapembe yote ya watu waovu;
lakini ataotesha mapembe ya watu wa haki.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.