Yona 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Kisha, Yawe akaamuru samaki mukubwa amumeze Yona, naye akabaki ndani ya tumbo la samaki huyo kwa muda wa siku tatu, usiku na muchana.

Maombi ya Yona

2Basi, Yona akiwa ndani ya tumbo la samaki yule, akamwomba Yawe Mungu wake,

3akisema:

Kwa sababu ya taabu yangu,

nilikuomba, ee Yawe,

nawe ukanisikiliza;

toka chini kuzimu, nilikulilia,

nawe ukasikiliza kilio changu.

4Ulinitupa katika kilindi, katikati ya bahari,

maji mengi yakanizunguka,

mawimbi na maji mengi vikapita juu yangu.

5Nilizani kwamba nimetupwa mbali nawe;

nisiweze kuliona tena hekalu lako takatifu.

6Maji yalinizunguka na kunisonga;

kilindi kilinifikia kila upande,

majani ya bahari yakanifunika kichwa.

7Niliteremuka mpaka kwenye misingi ya milima,

katika inchi ambayo milango yake imefungwa milele.

Lakini wewe, ee Yawe, Mungu wangu,

umenipandisha nikiwa muzima kutoka mule ndani ya shimo.

8Roho yangu ilipoanza kunitoka,

nilikukumbuka, ee Yawe,

maombi yangu yakakufikia

katika hekalu lako takatifu.

9Watu wanaoabudu sanamu za miungu ya bure,

wanautupilia mbali uaminifu wao kwako.

10Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,

nitakutolea sadaka,

na kutimiza viapo vyangu.

Yawe, ndiye anayeokoa.

11Basi, Yawe akamwamuru yule samaki, naye akamutapika Yona kwenye inchi kavu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help