1Katika siku makumi mbili na moja, mwezi wa saba mwaka uleule, neno la Yawe lilifika kwa njia ya nabii Hagai na kusema hivi:
2Sema na mutawala wa Yuda, Zerubabeli mwana wa Saltieli, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki na watu waliorudi kutoka katika uhamisho uwaambie hivi:
3Ni nani kati yenu anayekumbuka jinsi nyumba hii ilivyokuwa yenye utukufu? Sasa munaiona namna gani? Bila shaka sasa munaiona kama si kitu.
6Yawe wa majeshi anasema hivi: Kisha muda kidogo nitazitikisa mbingu na dunia, bahari na inchi kavu.
14Hagai akajibu na kusema hivi: Hivi ndivyo inavyokuwa kwa watu wa taifa hili mbele yangu –ni ujumbe wa Yawe– na kila kitu wanachofanya; hata vitu wanavyotoa kwenye mazabahu ni vichafu.
15Lakini sasa mufikiri vizuri juu ya mambo yatakayotukia. Mbele ya kuanza kujenga upya nyumba yangu,
16hali yenu ilikuwa namna gani? Mutu alifika kwenye fungu la ngano akingojea kupata vipimo makumi mbili, lakini kulikuwa vipimo kumi tu. Mutu alifika kwenye mutungi wa divai akingojea kujaza vyombo makumi tano, lakini kulikuwa makumi mbili tu.
17Mimea yenu yote muliyojaribu kupanda, niliiharibu kwa kuikausha na kwa kuipiga kwa ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo hamukunirudilia.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
18Sasa, mufikiri vizuri juu ya mambo yatakayotukia. Leo ni siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kenda, siku ambayo musingi wa hekalu umekamilika. Basi mufikiri vizuri:
19Ingawa sasa hakuna ngano ndani ya gala, nayo mizabibu, tini, mikomamanga na mizeituni haijazaa kitu, lakini tangu leo, nitawabariki.
Ahadi kwa Zerubabeli20Siku ileile ya makumi mbili na ine, mwezi wa kenda, neno la Yawe lilimufikia Hagai kwa mara ya pili kusema hivi:
21Sema na Zerubabeli mutawala wa Yuda umwambie hivi: Nitazitikisa mbingu na dunia
22na kuangusha falme na kukomesha nguvu zao. Nitayapindua magari yao ya vita na waaskari wapanda-farasi wake, nao wataanguka na kuuana wao kwa wao.
23Siku hiyo, nitakutwaa wewe Zerubabeli mwana wa Saltieli, mutumishi wangu.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!
Nitakusimika utawale kwa jina langu.
–Ni ujumbe wa Yawe!
Wewe ndiwe niliyekuchagua.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.