Hesabu 24 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Sasa Balamu akatambua kwamba Yawe alipenda kuwabariki Waisraeli, kwa hiyo hakukwenda sawa vile mara ingine kwa kutafuta uchawi. Akaelekea kwenye jangwa,

2akainua macho, akawaona Waisraeli wamepiga kambi kila kabila pahali pake. Kisha Roho ya Mungu ikamufikia,

3naye akasema mashairi haya ya Yawe:

Mashairi yangu mimi Balamu mwana wa Peori

mashairi ya mutu aliyefumbuliwa macho.

4Anasema yeye aliyesikia maneno ya Mungu,

mutu aliyeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu,

mutu anayeinama uso mpaka chini na kuona wazi.

5Hema zenu zinapendeza sana, enyi watu wa Yakobo;

hakika, kambi zenu, enyi watu wa Israeli!

6Ni kama mabonde yanayotiririka maji,

kama bustani kandokando ya muto,

kama miti ya mishubiri Yawe aliyopanda,

kama mierezi kandokando ya maji.

7Watakuwa na hazina ya kutosha ya maji,

mbegu yao itapata maji mengi,

mufalme wao atakuwa mukubwa kuliko Agagi,

na ufalme wake utatukuka sana.

8Mungu aliwaondoa kutoka Misri,

naye anawapigania kwa nguvu kama mbogo.

Atayateketeza mataifa yanayokuwa waadui zao,

atavunjavunja mifupa yao,

atawachoma kwa mishale yake.

9Atavizia na kulala chini kama simba,

nani atasubutu kumwamusha?

Abarikiwe yeyote atakayekubariki wewe Israeli,

alaaniwe yeyote atakayekulaani.

10Balaki akawaka hasira juu ya Balamu, akapiga mikono kwa kasirani na kumwambia: Nilikuita uwalaani waadui zangu, lakini mara hizi zote tatu umewabariki!

11Sasa! Kwenda zako. Nilikuwa nimekuahidi kukupa zawadi nyingi, lakini Yawe hakukujalia kupata zawadi hizo, amekunyima!

12Balamu akamujibu Balaki: Unakumbuka nilivyowaambia wajumbe uliowatuma kwangu.

13Niliwaambia kwamba hata kama ungenipa nyumba yako imejaa feza na zahabu, mimi sitaweza kubadilisha agizo la Yawe, kwa kufanya jambo lolote, jema au baya kwa mapenzi yangu mwenyewe. Nilisema kwamba atakachosema Yawe ndicho nitakachosema.

14Sasa ninarudi kwa watu wangu, lakini mbele sijaondoka, acha nikuambie mambo ambayo watu hao watawatendea watu wako siku zinazokuja.

15Basi, Balamu akasema mashairi haya:

Mashairi yangu mimi Balamu mwana wa Beori,

mashairi ya mutu aliyefumbuliwa macho,

16mashairi ya mutu aliyesikia maneno ya Mungu,

na mutu anayejua maarifa ya Mungu Mukubwa,

mutu anayeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu,

mutu anayeinama uso mpaka chini, macho wazi.

17Ninamwona atakayekuja,

ninamwona, lakini hayuko karibu.

Nyota itatokea kwa wazao wa Yakobo,

atatokea mufalme kati ya Waisraeli.

Kwa fimbo yake atapiga viongozi wa Wamoabu,

atawaangamiza wazao wote wa Seti.

18Edomu itakuwa urizi wake,

Seiri itakuwa mali yake,

Israeli itapata ushindi mukubwa.

19Mumoja wa wazao wa Yakobo atatawala

naye atawaangamiza watakaobaki katika muji.

20Kisha Balamu akawaangalia Waamaleki, akatoa mashairi haya:

Amaleki ni taifa lenye nguvu kuliko yote,

lakini kwa mwisho litaangamia kabisa.

21Kisha Balamu akawaangalia Wakeni, akatoa mashairi haya:

Makao yenu ni salama, enyi Wakeni,

kama chicha juu kabisa ya mulima.

22Lakini mutateketezwa, enyi Wakeni.

Mutapelekwa mateka na Asuria mpaka wakati gani?

23Tena Balamu akatoa mashairi haya:

Ole! Nani ataishi Mungu atakapofanya hayo?

24Mashua zitafika kutoka Kitimu,

wataishambulia Asuria na Eberi,

lakini nao vilevile wataangamia milele.

25Basi, Balamu akaondoka, akarudi kwake; Balaki vilevile akaenda zake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help