1“Na kisha kufika na kurizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu anawapa ikuwe yenu na kuishi huko,
2utatwaa malimbuko ya mazao utakayovuna katika inchi Yawe, Mungu wenu, anayokupa, na kuyaweka katika kikapu mpaka pale pahali ambapo Yawe, Mungu wenu, amechagua pawe makao yake.
3Utamwendea kuhani anayetumika wakati huo, na kumwambia: ‘Leo ninashuhudia mbele ya Yawe, Mungu wangu, kwamba nimeingia katika inchi aliyowaapia wazee wetu kwamba atatupatia’.
4“Naye kuhani atakapotwaa kikapu hicho toka mikono yako na kukiweka mbele ya mazabahu ya Yawe, Mungu wako,
5utasema maneno haya mbele ya Yawe, Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Musuria aliyetangatanga huko na huko, kisha akashuka kwenda Misri akaishi huko kama mugeni. Yeye na jamaa yake walikuwa watu wachache tu walipokuwa huko, lakini wakakuwa taifa kubwa lenye nguvu na watu wengi.
6Wamisri walitutendea kwa ukali wakatutesa na kutulazimisha kufanya kazi ngumu ya watumwa.
7Kisha tukamulilia Yawe, Mungu wa wazee wetu, akasikia kilio chetu, na kuona mateso yetu, kazi ngumu na mateso tulizozipata.
8Basi, Yawe akatutoa huko Misri kwa mukono wake wa nguvu ulionyooshwa, kwa vitisho, vitambulisho na maajabu.
9Akatuleta hapa na kutupatia inchi hii inayotiririka maziwa na asali.
10Na sasa ninamuletea Yawe malimbuko ya mazao ya inchi ambayo amenipa’.
“Kisha utaweka kikapu chini, mbele ya Yawe, Mungu wako, na kuabudu mbele yake.
11Nawe utafurahia mema yote ambayo Yawe, Mungu wako, amekujalia wewe na jamaa yako. Nao watafurahi pamoja nawe.
12Kila nyuma ya miaka mitatu, kila mumoja wenu atatoa sehemu ya kumi ya mazao yake yote kwa ajili ya Walawi na wageni, wayatima na wajane, kusudi wapate chakula chote wanachohitaji wanapokuwa katika miji yenu.
13Kisha utasema mbele ya Yawe, Mungu wako, hivi: ‘Nimetoa katika nyumba yangu fungu takatifu, nikawapa Walawi, wageni, wayatima na wajane, kama vile ulivyoniamuru nifanye. Sijavunja amri zako wala sijasahau.
14Sikukula sehemu ya kumi yoyote nilipokuwa ninaomboleza; sikuitoa inje ya nyumba yangu nilipokuwa muchafu na sikutoa sehemu ya kumi hiyo kwa wafu. Nimekutii ee Yawe, Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoamuru juu ya sehemu ya kumi.
15Uangalie chini kutoka makao yako matakatifu mbinguni, uwabariki watu wako Israeli na inchi uliyotupatia kama vile ulivyowaapia wazee wetu; inchi inayotiririka maziwa na asali’.
Watu wa Yawe16“Leo hii, Yawe, Mungu wenu, anawaamuru kushika masharti na maagizo haya. Mukuwe waangalifu kuyatimiza kwa moyo wote na roho yote.
17Leo Yawe ameahidi kwamba atakuwa Mungu wenu, kama mutafuata njia zake na kushika masharti, amri, na maagizo yake na kutii sauti yake.
18Nanyi mumeahidi kwamba mutakuwa watu wake yeye mwenyewe na kwamba mutashika amri zake zote.
19Atawafanya ninyi kuwa taifa kubwa kuliko mataifa yote aliyoumba. Nanyi mutatetea jina lake, sifa yake na heshima yake. Ninyi mutakuwa watakatifu wake kama vile alivyosema.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.