1Mimi ni mutu niliyepata mateso
kwa fimbo ya kasirani ya Mungu.
2Amenikamata na kunitembeza
katika giza ambako hakuna mwangaza.
3Amenyoosha mukono wake juu yangu mimi tu,
akiniazibu tena na tena muchana kutwa.
4Amenichakalisha ngozi na nyama,
ameivunja mifupa yangu.
5Amenikusanyia na kunizungushia
uchungu na mateso.
6Amenikalisha katika giza
kama watu waliokufa zamani.
7Amenizungushiia ukuta na siwezi kutoka,
amenifunga kwa minyororo mizito.
8Ingawa ninaita na kuomba musaada
anazuiza maombi yangu yasimufikie.
9Amezifunga njia zangu kwa mawe makubwa,
amepotosha mapito yangu.
10Alikuwa kwangu kama dubu anayevizia,
kama simba katika maficho.
11Alinifukuza katika njia yangu,
akanirarua na kuniacha ukiwa.
12Aliuvuta upinde wake,
akanielekezea mushale wake.
13Alinichoma ndani ya moyo kwa mishale,
kutoka katika kifuko chake.
14Nimekuwa kitu cha kuchekelewa kwa watu wote,
muchana kutwa nimekuwa mutu wa kuzomewa.
15Amenijaza taabu,
akanishibisha uchungu.
16Amenisagisha meno katika mawe,
akanifanya nigaegae katika majivu.
17Moyo wangu haujui tena amani,
nimesahau furaha.
18Nimewaza: Nimekata tamaa kabisa,
tumaini langu kwa Yawe limetoweka.
19Kukumbuka taabu na kutangatanga kwangu
kunanipa uchungu na sumu.
20Ninafikiri juu ya hayo siku zote,
nayo roho yangu imejaa huzuni.
21Lakini ninakumbuka jambo hili moja,
nami ninakuwa na tumaini:
22Wema wa Yawe haukomi,
huruma zake hazina mwisho.
23Uaminifu wake ni mukubwa sana,
kila mara kunapokucha ni mupya kabisa.
24Yawe ndiye sehemu yangu,
hivyo nitamuwekea tumaini langu.
25Yawe ni muzuri kwa wanaomutegemea,
kwa wote wanaomutafuta.
26Ni vizuri kwa mutu kungojea kwa utulivu
wokovu unaotoka kwa Yawe.
27Ni vizuri kwa mutu kujifunza uvumilivu
tangu wakati wa ujana wake.
28Heri kwa mutu kukaa peke yake na kimya,
mambo mazito yanapomupata kutoka kwa Mungu.
29Inamupasa kuinama na kujinyenyekeza,
labda tumaini litakuwa likingali.
30Inamupasa kumugeuzia shavu mwenye kumupiga,
na kuwa tayari kupokea matusi yake.
31Yawe hatatutupilia milele.
32Ingawa atatufanya tuhuzunike,
atakuwa na huruma tena,
kadiri ya wingi wa wema wake.
33Yeye hapendelei kuwatesa
wala kuwahuzunisha wanadamu.
34Wafungwa wote katika inchi
wanapoteswa na kupondwa,
35haki za wanadamu zinapopotoshwa
mbele ya Mungu Mukubwa,
36wanapomunyima mutu haki katika tribinali,
basi, Yawe haoni hayo?
37Nani anayeweza kusema kusudi kitu kifanyike
ikiwa Yawe asipoamuru ikuwe hivyo?
38Maovu na mema yanatokea tu
kwa amri ya Mungu Mukubwa.
39Kwa nini mutu anungunike
ikiwa ameazibiwa kwa ajili ya zambi zake?
40Tupime na kuchunguza mwenendo wetu
tupate kumurudilia Yawe.
41Tumufungulie Mungu mioyo yetu
na kumwomba kule juu mbinguni:
42Tulikukosea na kukuasi,
nawe haujatusamehe bado.
43Umejifunika hasira yako na kutufuatilia,
ukatuua bila huruma.
44Umejifunika wingu
kusudi maombi yoyote yasipite.
45Umetufanya kuwa takataka na uchafu
kati ya mataifa.
46Waadui zetu wote wanatuzomea.
47Woga na hofu vimetuandama
tumepatwa na uharibifu na maangamizi.
48Macho yangu yanabubujika mito ya machozi
kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu.
49Macho yangu yanatelemusha machozi bila kukoma,
50mpaka Yawe kutoka kule mbinguni
aangalie chini na kuona.
51Ninahuzini sana kuona
yale yaliyowapata wabinti wa muji wangu.
52Nimewindwa kama ndege
na hao wanaonichukia bila sababu.
53Walinitupa ndani ya shimo nikiwa muzima
na juu yangu wakalundika mawe.
54Maji yalianza kunifunika kichwa,
nami nikafikiri: Huu ni mwisho wangu.
55Kutoka chini ndani ya shimo,
nilikulilia ee Yawe.
56Wewe umenisikia nikikulilia:
Usiache kusikiliza maombi yangu ya musaada.
57Nilipokuita ulifika karibu nami
ukaniambia: Usiogope!
58Ulinitetea katika maneno yangu, ee Yawe,
uliyakomboa maisha yangu.
59Uliuona uovu niliotendewa, ee Yawe;
uniamulie kwa wema maneno yangu.
60Umeuona uovu wa waadui zangu,
na mipango yao yote juu yangu.
61Umesikia matukano yao, ee Yawe,
na mipango yao yote juu yangu.
62Maneno na mawazo ya waadui zangu siku nzima,
ni juu ya kuniangamiza mimi.
63Wakiikaa au wakienda,
ni mimi ndiye wanayemuzomea.
64Uwalipize, ee Yawe,
sawasawa na matendo yao,
sawasawa na kazi ya mikono yao.
65Uifanye mioyo yao kuwa migumu,
na laana yako iwashukie.
66Uwafuatilie kwa hasira na kuwaangamiza
toka katika dunia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.