1Walipokwisha kukamata mupango wa kutusafirisha kwa njia ya chombo mpaka Italia, wakamuweka Paulo na wafungwa wengine chini ya uangalizi wa mukubwa mumoja wa waaskari aliyeitwa Yulio. Yeye alikuwa wa kundi la waaskari lililoitwa “Kundi la waaskari wa mufalme.”
2Tukapanda ndani ya chombo kilichotoka Adramiti, kilichokuwa tayari kupitia kwenye vivuko vya jimbo la Azia. Halafu tukaondoka tukiwa pamoja na mwanainchi mumoja wa Makedonia aliyeitwa Aristarko, wa Tesalonika.
3Kesho yake tukatua Sidona. Yulio aliyemutendea Paulo mema, akamupa ruhusa ya kwenda kuonana na warafiki zake, wapate kumupa vitu alivyohitaji.
4Kutoka kule, tukapita pembenipembeni ya kisanga cha Kipuro kwa kuepuka upepo uliokuwa ukivuma tokea mbele yetu.
5Tukavuka bahari upande wa jimbo la Kilikia na Pamfilia, na kufika katika muji Mira, wa jimbo la Likia.
6Kule yule mukubwa wa waaskari akakuta chombo kilichotoka Alesanduria kwa kwenda Italia, naye akatupandisha ndani yake.
7Tukasafiri polepole muda wa siku nyingi na kwa shida sana tukafika karibu na muji Kinido. Na kwa sababu upepo ulituzuiza kuendelea mbali ngambo ile, tukapita upande wa kusini wa kisanga cha Krete, kuelekea Salmone.
8Tuliendelea pembenipembeni yake kwa shida sana hata tukafika pahali panapoitwa “Vivuko Vizuri,” karibu na muji Lasea.
9Kisha kupitisha siku nyingi, tukafikia katika nyakati za hatari za safari ya bahari, kwa maana siku ya kufunga kula ilikuwa imekwisha kupita. Halafu Paulo akatupatia shauri hili:
10“Wanaume, ninaona kwamba safari yetu itakuwa ya hatari na hasara nyingi, si kwa chombo na mizigo tu, lakini kwa maisha yetu vilevile.”
11Lakini yule mukubwa wa waaskari akasadiki zaidi maneno ya kapiteni na ya mwenye chombo kuliko kufuata shauri la Paulo.
12Na kwa sababu kivuko kile hakikukuwa na nafasi zuri ya kukaa wakati wa baridi kali, watu wengi kati yetu wakakubaliana kuondoka kule, kusudi ikiwezekana wafike Foinike, na kupitishia wakati wa baridi kali kule. Foinike ni kivuko kimoja kinachokuwa katika kisanga cha Krete, kinachoelekea upande wa kaskazini-magaribi na wa kusini-magaribi.
Zoruba katika bahari13Upepo usiokuwa mukali ulipoanza kuvuma tokea kusini, wakazani kwamba wataweza tu kutimiza sawa walivyokuwa wamekusudia. Wakapandisha nanga na kuendelea pembenipembeni karibu sana na Krete.
14Lakini nyuma kidogo, upepo mukali sana wa zoruba unaotokea upande wa mashariki-kaskazini ukavuma ukishuka tokea kwenye kisanga.
15Upepo ukapeleka chombo, nacho hakikuweza kushindana nao. Halafu tukakiacha tu kipelekwe na upepo.
16Tulipokuwa tukipita upande wa kusini wa kisanga kidogo kinachoitwa Kauda, tuliweza kwa shida sana kuopoa mutumbwi unaokokotwa na chombo.
17Watumishi wa chombo walipokwisha kunyanyulia mutumbwi ule ndani ya chombo, wakakaza chombo kwa kukifungafunga na kamba kwa kukikingia na nguvu ya upepo. Na kwa kuwa waliogopa kwamba wasikwame kwenye lundo la muchanga wa ngambo ya Sirti, wakashusha tanga na kuachilia chombo kipelekwe na upepo.
18Kesho yake kwa kuona jinsi zoruba ilivyoendelea kutusukumasukuma kwa nguvu, wakaanza kutupa mizigo katika bahari.
19Na siku iliyofuata wakaamua kutupa hata vifaa vya chombo.
20Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona tena jua wala nyota, nayo zoruba ikaendelea kuvuma kwa nguvu. Kwa mwisho tukakata kitumaini chote cha kupona.
21Watu walikuwa wamepitisha siku nyingi bila kula kitu. Halafu Paulo akasimama mbele yao na kusema: “Warafiki zangu, mungefuata shauri langu na kutoondoka Krete, hamungepata hasara hii na kupoteza vitu kama hivi.
22Sasa ninawaomba mujipe moyo, kwa maana hakuna hata mumoja kati yenu atakayekufa, chombo tu ndicho kitakachoharibika.
23Kwa maana usiku malaika wa Mungu, ninayekuwa mutu wake na ninayemwabudu, alinitokea
24na kuniambia: ‘Paulo, usiogope! Sherti usambe mbele ya Mufalme wa Roma. Na tena kwa kuwa inamupendeza Mungu kukutendea mema, yeye ataokoa maisha ya watu hawa wote wanaosafiri pamoja nawe.’
25Basi mujipe moyo, kwa sababu ninamutumainia Mungu kwamba itatendeka sawasawa nilivyoambiwa.
26Lakini ni sherti tutupwe kwenye kisanga kimoja.”
27Tulieneza majuma mawili tukipelekwa huku na huko na zoruba katika bahari ya Adria. Katikati ya usiku watumishi wa chombo waliwazia kwamba tumekaribia inchi kavu.
28Wakashusha kipimo ndani ya maji nao wakapata metre makumi ine kwenda chini. Mbali kidogo wakatupa tena kipimo na kupata metre makumi tatu.
29Kwa kuogopa kwamba chombo kisikwame kwenye mawe, wakashusha nanga ine za upande wa nyuma wa chombo na kungojea usiku ukuche.
30Wabaharia walitafuta kukimbia toka ndani ya chombo, wakashusha mutumbwi katika bahari, wakisema kwamba wanataka kufunga nanga tokea upande wa mbele.
31Lakini Paulo akamwambia yule mukubwa wa jeshi pamoja na waaskari wengine: “Watu hawa wasipobakia ndani ya chombo hamutaokolewa.”
32Halafu waaskari wakakata kamba zilizofunga ule mutumbwi na kuachilia uanguke katika bahari.
33Usiku ulipokaribia kucha, Paulo akawasihi watu wote kula chakula, akisema: “Sasa leo ni siku ya kumi na ine tangu mulipobaki bila kula kitu chochote.
34Basi ninawasihi ninyi mukule chakula, kwa sababu kitawafalia kusudi musikufe. Kwa maana hakuna mumoja kati yenu atakayepatwa na hasara yoyote hata kidogo.”
35Kisha kusema maneno hayo, Paulo akatwaa mukate, akamushukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, na akaanza kula.
36Halafu wote wakatiwa moyo tena, nao vilevile wakakula chakula.
37Kwa jumla tulikuwa watu mia mbili na makumi saba na sita ndani ya chombo.
38Walipokwisha kushiba, wakatupa mizigo ya ngano katika bahari kwa kupunguza uzito wa chombo.
Chombo kinavunjika39Kulipokucha wabaharia hawakutambua inchi ile lakini wakaona nafasi bahari inapoingia ndani ya inchi kavu na kwenye kivuko. Basi wakakusudia kwenda kukwamisha chombo kule, kama ikiwezekana.
40Wakafungua nanga na kuziachilia zizame ndani ya bahari. Vilevile waliregeza kamba za makasia ya kuongoza chombo. Kisha wakafunga tanga ndogo mbele ya chombo kusudi kipelekwe na upepo, nao wakaelekea kwenye kile kivuko.
41Lakini wakakwama kwenye lundo ya muchanga na chombo kikakwama pale. Sehemu ya mbele ya chombo ikazama kabisa pasipo kutikisika, lakini sehemu ya nyuma ikavunjikavunjika kwa kupigwa na zoruba kwa nguvu.
42Halafu waaskari wakapata wazo la kuwaua wafungwa, kusudi hata mutu mumoja kati yao asitoroke kwa kuogelea.
43Lakini kwa kuwa mukubwa wa jeshi alitaka kumuponyesha Paulo, yeye akawazuiza wasitimize kusudi lao. Akaamuru wale waliojua kuogelea wajitupe wa kwanza ndani ya maji na kuvuka mpaka inchi kavu.
44Nao wengine wawafuate wakikamatilia kwenye mbao au kwenye vipande vya chombo. Ni vile watu wote walivyofika inchi kavu salama.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.