1Nyuma ya muda fulani, wakati wa mavuno ya ngano, Samusoni akatwaa mwana-mbuzi, akaenda kumutembelea muke wake. Akamwambia baba mukwe wake kwamba anataka kumwona muke wake ndani ya chumba chake. Lakini baba mukwe hakumuruhusu,
2akamwambia: “Mimi nilizani kwamba ulimuchukia kabisa. Kwa hiyo nilimwoesha kwa rafiki yako. Hata hivyo, dada yake mudogo ni muzuri kuliko yeye. Tafazali, umwoe huyo kwa pahali pake.”
3Samusoni akamwambia: “Mara hii sitakuwa na kosa kwa yale nitakayowatendea Wafilistini.”
4Basi, Samusoni akaenda, akawakamata mbweha mia tatu naye akawafunga mikia yao pamoja wawili wawili. Kisha akaweka mwenge katika kila mbweha wawili wawili.
5Halafu akaiwasha hiyo mienge na kuwaachilia. Wakaingia kwenye mashamba ya Wafilistini na kuteketeza miganda ya ngano na vilevile ngano iliyokuwa bado haijavunwa hata na mashamba ya mizeituni.
6Wafilistini walipotaka kujua aliyefanya hayo, waliambiwa: “Ni huyo Samusoni, mukwe wa Mutimuna, ndiye amefanya hivyo kwa sababu huyo baba mukwe wake ametwaa muke wake na kumwoesha kwa kijana mumoja aliyekuwa rafiki ya Samusoni mwenyewe katika arusi.” Basi Wafilistini wakaenda kumuchoma kwa moto yule mwanamuke pamoja na baba yake.
7Samusoni akawaambia hao Wafilistini: “Kama hayo ndiyo muliyofanya, ninaapa kwamba sitaondoka mpaka nimelipiza kisasi.”
8Basi, akawashambulia vikali na kuwaua wengi. Kisha akaenda kuishi katika pango la Etamu lililokuwa chini ya jiwe.
Samusoni anawashinda Wafilistini9Wafilistini wakakuja, wakapiga kambi yao katika inchi ya Yuda na kuushambulia muji wa Lehi.
10Watu wa Yuda wakawauliza: “Kwa nini mumekuja kutushambulia?” Nao wakawajibu: “Tumekuja kusudi tumufunge Samusoni na kumutendea kama alivyotutendea.”
11Basi, watu elfu tatu wa Yuda wakamwendea Samusoni katika pango chini ya jiwe la Etamu wakamwambia: “Haujui kwamba Wafilistini wanatawala juu yetu? Angalia basi, jambo ulilotutendea!”
Samusoni akawajibu: “Kama walivyonitendea ndivyo nilivyowatendea.”
12Wakamwambia: “Tumekuja kukufunga kusudi tukutie katika mikono yao.”
Samusoni akawaambia: “Muniapie kwamba ninyi wenyewe hamutaniua.”
13Nao wakamwambia: “Sisi hatutakuua lakini tutakufunga tu na kukutia katika mikono yao.” Basi, wakamufunga kwa kamba mbili mupya na kumutosha inje ya pango.
14Alipofika Lehi, Wafilistini wakamwendea mbio na walikuwa wanapiga kelele. Kwa rafla roho wa Yawe akamushika Samusoni kwa nguvu na zile kamba walizomufunga kwenye mikono yake zikakatika kama kitani kilichoguswa na moto, navyo vifungo vikaanguka chini.
15Samusoni akaona mufupa mubichi wa taya ya punda, akautumia kuwaua watu elfu moja.
16Kisha Samusoni akasema:
“Kwa utaya wa punda,
nimeua watu elfu moja.
Kwa utaya wa punda,
nimekusanya malundo ya maiti.”
17Alipomaliza kusema, akatupa utaya huo. Pahali pale pakaitwa Ramati-Lehi, maana yake “Mulima wa Utaya”.
18Kisha Samusoni akashikwa na kiu sana. Basi, akamwomba Yawe, akisema: “Ee Mungu, wewe ndiwe uliyeleta ukombozi huu, kwa kunitumia mimi mutumishi wako. Sasa utaniacha nikufe kwa kiu na kutekwa na Wafilistini hawa wasiotahiriwa?”
19Mungu akafungua pahali palipokuwa shimo kule Lehi, akatiririsha maji. Samusoni akakunywa maji hayo na nguvu zake zikamurudilia. Chemichemi hiyo ikaitwa “Kisima cha Yule Anayeita” nayo iko kule Lehi mpaka leo.
20Samusoni akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kwa miaka makumi mbili, nyakati za Wafilistini.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.