1Yesu aliposhuka toka kwa mulima, makundi mengi ya watu wakamufuata.
2Halafu mutu mumoja mwenye ukoma akakuja, akapiga magoti mbele yake na kumwambia: “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”
3Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!”
Na mara moja mutu yule akatakaswa ukoma wake.
4Kisha Yesu akamwambia: “Angalisho, usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”
Yesu anaponyesha mutumishi wa mukubwa wa waaskari(Lk 7.1-10)5Yesu alipokuwa akiingia katika muji Kapernaumu, mukubwa mumoja wa waaskari akamufikia na kumusihi,
6akisema: “Bwana, mutumishi wangu anawezwa na ugonjwa wa kupooza, naye amelala ndani ya nyumba, akiteswa sana.”
7Yesu akamwambia: “Nitakuja kumuponyesha.”
8Lakini yule mukubwa akamujibu: “Bwana, mimi sistahili kukupokea ndani ya nyumba yangu. Lakini uamuru kwa neno tu na mutumishi wangu atapona.
9Hata mimi vilevile ni mutu mwenye kuwa chini ya mamlaka ya wakubwa, na tena nina waaskari wengine wanaokuwa chini yangu. Nami nikimwambia mumoja: ‘Kwenda!’, naye anakwenda. Nikimwambia mwingine: ‘Kuja!’, naye anakuja. Na nikimwambia mutumishi wangu: ‘Fanya hivi!’, naye anafanya vile.”
10Yesu aliposikia maneno haya, akashangaa na kuwaambia watu waliomufuata: “Kweli ninawaambia: katika inchi yote ya Israeli, sijaona bado mutu anayekuwa na imani kubwa kama huyu.
11Ninawaambia wazi kwamba watu wengi watakuja toka mashariki na magaribi, nao watachangia meza pamoja na Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwenye karamu katika Ufalme wa mbinguni.
12Lakini wale waliopaswa kushiriki katika Ufalme ule watatupwa inje kwenye giza, na kule watalia na kusaga meno.”
13Kisha Yesu akamwambia yule mukubwa wa waaskari hivi: “Urudie kwako, na ifanyike kwako sawa ulivyoamini.”
Na saa ile ile mutumishi wake akapona.
Yesu anaponyesha wagonjwa wengi(Mk 1.29-34; Lk 4.38-41)14Kisha Yesu akafika kwa nyumba ya Petro, na mule akamukuta mama mukwe wa Petro amelala katika kitanda na ugonjwa wa homa.
15Yesu akamugusa mukono, naye akapona homa. Halafu mama yule akasimama na kuanza kumushugulikia.
16Na ilipokuwa magaribi, wakamuletea Yesu watu wengi waliokuwa na pepo. Naye akawafukuza wale pepo akiwaamuru kwa neno tu na kuwaponyesha wagonjwa wote.
17Alifanya hivi kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Isaya: “Yeye alitwaa uzaifu wetu, naye amebeba muzigo wa magonjwa yetu.”
Namna ya kumufuata Yesu(Lk 9.57-62)18Yesu alipoona kundi la watu wakimuzunguka, akatoa amri ya kuvuka ngambo ingine ya ziwa.
19Mwalimu mumoja wa Sheria akamufikia na kumwambia: “Mwalimu, nitakufuata popote utakapokwenda.”
20Yesu akamujibu: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu, nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”
21Na mutu mwingine mumoja kati ya wanafunzi wake akamwambia: “Bwana, unipe ruhusa kwanza niende kuzika baba yangu.”
22Lakini Yesu akamujibu: “Unifuate mimi, uwaache hao wafu wazike wafu wao.”
Yesu anatuliza zoruba(Mk 4.35-41; Lk 8.22-25)23Halafu Yesu akaingia ndani ya chombo, nao wanafunzi wake wakaenda naye.
24Mara moja zoruba kubwa ikatokea katika ziwa na maji yakajitupatupa ndani ya chombo. Lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.
25Wanafunzi wake wakamujongelea, wakamwamusha na kumwambia: “Bwana, utuokoe! Tunakufa!”
26Yesu akawajibu: “Sababu gani munaogopa kama hivi? Hakika imani yenu ni ndogo!” Halafu akasimama, akakaripia zoruba na maji na kukakuwa kimya kabisa ndani ya ziwa.
27Nao wakashangaa, wakisema: “Huyu ni mutu gani, hata zoruba na ziwa vinamutii?”
Yesu anaponyesha watu wawili wenye pepo(Mk 5.1-20; Lk 8.26-39)28Yesu alipofika ngambo ingine ya ziwa la Galilaya, katika inchi ya Wagedari, watu wawili wenye pepo wakamufikia, wakitoka kwenye makaburi. Watu wale walikuwa na pepo wakali sana, hata hakuna mutu aliyesubutu kupita katika njia ile.
29Halafu wakaanza kulalamika wakisema: “Kuna maneno gani kati yako na sisi wewe Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kwa kututesa mbele ya kutimia kwa wakati wetu?”
30Na karibu na pale kulikuwa kundi kubwa la nguruwe wakijitafutia chakula.
31Wale pepo wakamusihi Yesu wakisema: “Ikiwa unataka kutufukuza, ututume tuingie ndani ya wale nguruwe.”
32Na Yesu akawaambia: “Mwende!” Basi wakatoka ndani ya wale watu na kuingia ndani ya nguruwe. Mara moja kundi zima likatelemuka mbio toka kwenye maporomoko ya mulima na kujitupa ndani ya ziwa nao wakazama ndani ya maji.
33Wachungaji wa nguruwe wale wakaenda mbio katika muji kupasha habari za mambo yaliyotendeka na habari ya wale watu wawili waliokuwa na pepo.
34Basi watu wote wa muji wakatoka kwa kumufikia Yesu na wakati walipomwona wakamusihi aondoke katika inchi yao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.