1Yawe akamwambia Musa: “Kungali bado pigo moja nitakalomuletea mufalme wa Misri na inchi ya Misri. Kisha atawaacha muondoke hapa. Naye atakapowaacha muondoke, atawafukuza kwa lote.
2Uwaambie Waisraeli sasa wasikie vizuri kwamba kila mumoja wao, mwanaume na mwanamuke, anapaswa kumwomba jirani yake vyombo vya feza na zahabu.”
3Yawe akawafanya Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Wamisri. Tena, Musa mwenyewe akakuwa mutu mukubwa sana katika inchi ya Misri na mbele ya wakubwa na mufalme na watu wote.
4Musa akamwambia mufalme wa Misri: “Yawe anasema hivi: ‘Katikati ya usiku wa leo, nitapitia katikati ya inchi ya Misri.
5Nitakapopita, kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri atakufa, kuanzia muzaliwa wa kwanza wako wewe mufalme wa Misri ambaye ni murizi wako, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mujakazi anayesaga ngano kwa jiwe. Hata wazaliwa wa kwanza wa mifugo nao wote watakufa.
6Kutakuwa kilio kikubwa katika inchi yote ya Misri, kilio ambacho hakijapata kutokea, wala hakitatokea tena.
7Lakini kati ya Waisraeli hakuna hata imbwa atakayemufokea mutu wala nyama kusudi upate kutambua kwamba mimi Yawe ninaweka tofauti kati ya Waisraeli na Wamisri.’ ”
8Musa akamalizia kwa kumwambia mufalme: “Watumishi wako hawa watanifikia na kuinama mbele yangu kwa heshima, wakinisihi niondoke katika inchi ya Misri, mimi pamoja na watu wote wanaonifuata. Nyuma ya hayo, nitaondoka.” Kisha Musa, akiwa amekasirika, akaondoka kwa mufalme wa Misri.
9Yawe akamwambia Musa: “Mufalme wa Misri hatakusikiliza, kusudi maajabu yangu yapate kuongezeka katika inchi ya Misri.”
10Basi, Musa na Haruni walifanya maajabu hayo yote mbele ya mufalme wa Misri. Lakini Yawe alifanya moyo wa mufalme kuwa mugumu, akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke katika inchi yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.