Danieli 5 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Karamu ya mufalme Belsasari

1Siku moja mufalme Belsasari alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakubwa wake na kunywa divai pamoja nao.

2Kutokana na kunywa divai, mufalme Belsasari akatoa amri kwamba vile vyombo vya zahabu na feza ambavyo baba yake mufalme Nebukadneza alivyokamata kutoka hekalu la Yerusalema, viletwe kusudi avitumie kwa kunywea divai pamoja na wakubwa wake, wanawake wake na wahabara wake.

3Basi, vile vyombo vya zahabu na feza vilivyokamatwa katika hekalu kule Yerusalema vikaletwa. Mufalme, wakubwa wake, wanawake wake na wahabara wake wakavitumia kwa kunywea.

4Walikunywa na kusifu sanamu za miungu iliyotengenezwa na zahabu, feza, shaba, chuma, miti na mawe.

Maandiko juu ya ukuta

5Saa ileile, vidole vya mukono wa mwanadamu vikatokea na kuandika kwenye lipu ya ukuta wa nyumba ya kifalme uliopakaliwa chokaa pahali palipoangaziwa vizuri, mbele ya kinara cha taa. Mufalme aliuona mukono ule ukiandika.

6Basi, mufalme akabadilika rangi na kufazaika kwa ajili ya mawazo yaliyomufikia, viungo vyake vikaregea na magoti yakaanza kutetemeka.

7Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.

8Basi, wenye hekima wote wa mufalme wakakuja, lakini hawakuweza kuyasoma maandiko hayo wala kumujulisha mufalme maana yake.

9Basi, mufalme Belsasari akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakubwa wake wakakuwa na wasiwasi.

10Kutokana na kelele za mufalme na wakubwa wake, mama ya mufalme aliingia ndani ya chumba cha karamu, akasema: Uishi milele, ee mufalme! Si lazima mawazo yako yakufazaishe na rangi yako kubadilika.

11Katika ufalme wako kuna mutu ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake. Wakati wa utawala wa baba yako, mutu huyu alionekana kuwa mwenye ujuzi, ufahamu na hekima kama ya miungu. Baba yako, mufalme Nebukadneza, alimufanya kuwa mukubwa wa waaguzi, wachawi, Wakaldea wenye hekima, na waganga, Ang. 4.8

12kwa sababu ana roho njema, maarifa, ujuzi wa kufasiria ndoto, kufumbua mafumbo na kutatua matatizo. Jina la mutu huyo ni Danieli ambaye baba yako alimwita Beltesaza. Basi wamwite, naye atakuelezea maana ya maandiko haya.

Danieli anafafanua maandiko

13Basi, Danieli akaletwa mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: Wewe ndiwe Danieli, mumoja wa wafungwa ambao baba yangu mufalme, aliowaleta kutoka inchi ya Yuda?

14Nimesikia kwamba roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba una ujuzi, na akili, na hekima ya ajabu.

15Wenye hekima na wachawi walipoletwa hapa kusoma na kunielezea maana ya maandiko haya, walishindwa. Ang: 4.8

16Lakini, nimesikia kwamba wewe unaweza kueleza vitendawili na kutambua mafumbo. Basi, kama ukiweza kusoma maandiko haya na kunielezea maana yake, utavalishwa nguo nzuri ya rangi nyekundu na kuvalishwa mukufu wa zahabu katika shingo lako. Utapewa nafasi ya tatu katika ufalme huu.

17Danieli akamujibu mufalme Belsasari: Unaweza kubakia na zawadi zako, ee mufalme, au kumupa mutu mwingine. Hata hivyo, ee mufalme, nitakusomea maandiko hayo na kukuelezea maana yake.

18Ee mufalme, Mungu Mukubwa alimupa baba yako mufalme Nebukadneza ufalme, ukubwa, mamlaka na utukufu.

19Kwa sababu ya ukubwa aliomupa, watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote walitetemeka na kumwogopa. Nebukadneza aliweza kumwua mutu yeyote aliyetaka na kumwacha muzima mutu yeyote aliyetaka. Aliyetaka kumupandisha cheo alimupandisha, aliyetaka kumushusha cheo alimushusha.

20Lakini alipoanza kuwa na kiburi, akakuwa na roho ngumu na mwenye majivuno, aliondolewa katika kiti chake cha kifalme, akanyanganywa utukufu wake.

21Alifukuzwa mbali na wanadamu, akili yake ikafanywa kama ya nyama, akaishi na punda wa pori, akakuwa anakula majani kama ngombe, na kulowanishwa na umande wa mbinguni mpaka alipotambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.

22Lakini wewe Belsasari mwana wake, ingawa unayajua haya yote, haukujinyenyekeza!

23Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!

24Basi, Mungu ametuma mukono uandike maandiko haya.

25Maandiko yenyewe ni: MENE, MENE, TEKELI, PERESI.

26Na hii ndiyo maana yake.

MENE: Mungu amehesabu siku za ufalme wako na kuukomesha.

27TEKELI: wewe umepimwa kwenye mizani, nawe ukaonekana hauna uzito wowote.

28PERESI: ufalme wako umegawanywa kati ya Wamedi na Wapersi.

29Pale pale, mufalme Belsasari akaamuru kwamba Danieli avalishwe nguo nzuri nyekundu na mukufu wa zahabu katika shingo. Ikatangazwa kwamba Danieli atakamata sasa nafasi ya tatu katika ufalme. Ang. Mwa 41.42

30Usiku uleule, mufalme Belsasari wa Wakaldea, aliuawa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help