1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.
2Unisaidie,
ee Yawe!
Watu wema wamekwisha;
waaminifu wametoweka kati ya watu.
3Kila mumoja anamudanganya mwenzake;
anabembeleza lakini ni kwa moyo wa unafiki.
4Ee Yawe, ukomeshe midomo hiyo ya kudanganya,
na ndimi hizo zinazojigamba.
5Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda;
tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”
6Lakini Yawe anasema:
“Kwa sababu wamasikini wanaugua,
na wakosefu wanalia,
sasa ninasimama,
nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”
7Ahadi za Yawe ni safi,
safi kama feza iliyosafishwa katika chungu,
kama feza iliyosafishwa mara saba.
8Utulinde, ee Yawe,
utukinge siku zote na kizazi hiki kiovu.
9Waovu wanazunguka popote;
upotovu unatukuzwa kati ya watu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.