1Zaburi ya Daudi.
Yawe anamwambia bwana wangu:
“Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu
mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”
2Yawe ataeneza mamlaka yako kutoka Sayuni;
utatawala juu ya waadui zako wote.
3Watu wako watajitolea,
siku utakapokwenda kuwapiga waadui.
Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia,
kama umande unaotokeza asubui mapema.
4Yawe amekuapia hivi wala hatabadilisha nia yake:
“Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”
5Bwana wetu yuko karibu nawe;
atawaponda wafalme atakapokasirika.
6Atayahukumu mataifa na kuwaua watu wengi;
atawaponda waongozi kila nafasi katika dunia.
7Mufalme atakunywa maji ya kijito katika njia,
kisha atainua kichwa kwa ushindi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.