Zaburi 127 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Bila Mungu kazi ya mwanadamu haifai kitu

1Wimbo wa safari za kidini: wa Solomono.

Yawe asipoijenga nyumba,

wanaoijenga wanajisumbua bure.

Yawe asipoulinda muji,

wanaoulinda wanakesha bure.

2Munajisumbua bure kuamuka asubui mapema

na kuchelewa kwenda kupumzika magaribi,

mujipatie chakula kwa jasho lenu.

Mungu anatimiza mahitaji ya wapendwa wake hata wanapolala.

3Watoto ni urizi kutoka kwa Yawe;

uzao ni zawadi yake kwetu sisi.

4Watoto wanaokuwa na nguvu,

ni kama mishale katika mikono ya askari.

5Heri mutu anayekuwa na mishale hiyo kwa wingi.

Hatashindwa atakaposamba na waadui zake kwenye tribinali.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help