ZAKARIA 5 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maono ya sita: Kitabu kinachoruka

1Nilipoangalia tena niliona kitabu kinaruka katika anga.

2Yule malaika akaniuliza: Unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kitabu kinaruka katika anga; urefu wake ni metre kenda na upana wake ni metre ine na nusu.

3Basi, yeye akaniambia: Ndani ya kitabu hicho kumeandikwa laana ambayo inchi nzima itakayoipata. Upande mumoja imeandikwa kwamba wizi wote watafukuzwa katika inchi, na upande mwingine imeandikwa kwamba wote wenye kuapa uongo watafanyiwa vile vile.

4Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.

Maono ya saba: Mwanamuke ndani ya kikapu

5Yule malaika aliyeongea nami alinikaribia, akaniambia: Inua macho uone kile kinachokuja.

6Nami nikamwuliza: Ni kitu gani hicho? Naye akanijibu: Hicho ni kikapu chenye makosa ya inchi nzima.

7Kikapu chenyewe kilikuwa na mufuniko uliotengenezwa kwa chuma cha risasi; kilifunuliwa, nami nikaona mwanamuke ameikaa mule ndani.

8Yule malaika akaniambia: Mwanamuke yule ni mufano wa uovu! Kisha yule malaika akamusukumia ndani ya kikapu mwanamuke yule na kukifunika.

9Nilipoangalia, niliona wanawake wawili wanatokea; walikuwa wakirushwa na upepo, nao walikuwa na mabawa yenye nguvu kama ya korongo. Wanawake wale wakakiinua kile kikapu katika anga.

10Basi, nikamwuliza yule malaika aliyezungumuza nami: Wanakipeleka wapi kile kikapu?

11Naye akaniambia: Wanakipeleka katika inchi ya Sinari. Kule watakijengea hekalu na litakapokuwa tayari, watakiweka kikapu hicho ndani.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help