1Ewe mwanamuke unayekuwa muzuri sana,
amekwenda wapi yule mupenzi wako?
Ameelekea wapi mupenzi wako,
kusudi tupate kushirikiana nawe kwa kumutafuta?
Masemi ya muke2Mupenzi wangu amekwenda katika bustani yake,
pahali ambapo miti ya marasi inastawi.
Yeye anakulisha kondoo wake
na kukusanya mayungiyungi.
3Mimi ni wa mupenzi wangu, naye ni wangu;
yeye anawakulisha kondoo wake kwenye mayungiyungi.
Shairi la tanoMasemi ya mume4Mupenzi wangu, sura yako ni nzuri kama muji wa Tirza,
unapendeza kama Yerusalema,
unatisha kama jeshi lenye bendera.
5Usiniangalie, tafazali;
maana macho yako yananitisha.
Nywele zako ni kama kundi la mbuzi
wanaoshuka kwenye milima ya Gileadi.
6Meno yako ni kama kundi la kondoo dike
wanaotoka kwenye maji kisha kuogeshwa,
kila mumoja akiwa na pacha lake,
na hakuna yeyote aliyekufiwa.
7Mashavu yako ni kama nusu mbili za makomamanga
ndani ya ushungi wako.
8Kuna malkia makumi sita, wahabara makumi nane,
na wabinti wasiohesabika!
9Hakuna anayekuwa sawa njiwa yangu.
Anaenea kabisa.
Ni kipenzi cha mama yake,
ni binti wake pekee.
Wabinti wanamwangalia na kumwita mwenye heri,
nao malkia na wahabara wanaimba sifa zake.
10Ni nani huyu anayeonekana kama mapambazuko,
muzuri kama mwezi, mwenye kungaa kama jua,
na anatisha kama jeshi lenye bendera?
11Nimeingia katika bustani ya miti ya lozi,
kuangalia vichipukizi katika bonde,
kuona kama mizabibu imechanua,
na mikomamanga imechanua maua.
12Bila kutazamia, mupenzi wangu
akanitia katika gari la mukubwa.
WabintiWho We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.