1Sasa tuangalie mambo yanayoelekea zawadi za Roho Mutakatifu. Wandugu zangu, sitaki mukose kufahamu ukweli wa zawadi hizi.
2Munajua kwamba wakati mulipokuwa wapagani, mulikuwa mukivutwa na kupotoshwa na sanamu zisizosema.
3Kwa sababu hii ninataka mufahamu kwamba hakuna mutu ambaye anaongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema: “Yesu alaaniwe,” na hakuna mutu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana,” kama asipoongozwa na Roho Mutakatifu.
4Kuna zawadi mbalimbali, lakini ni Roho mumoja anayezitoa.
5Kuna utumishi wa namna mbalimbali, lakini ni Bwana mumoja ndiye wanayemutumikia.
6Kuna kazi za namna mbalimbali, lakini Mungu ni mumoja anayewezesha watu wote kuzitimiza.
7Na kwa kila mutu Roho anajifunua kwa faida ya wote.
8Basi mutu mumoja anapewa na Roho uwezo wa kusema maneno ya hekima, na mwingine uwezo wa kusema maneno ya ufahamu na Roho yule yule.
9Mwingine anapewa imani na Roho yule yule na mwingine uwezo wa kuponyesha wagonjwa.
10Mwingine anapewa uwezo wa kufanya miujiza, mwingine zawadi ya kutabiri, na mwingine uwezo wa kutambua roho ya uongo na Roho wa ukweli. Mwingine alipewa uwezo wa kusema luga za ajabu na mwingine uwezo wa kutafsiri luga zile.
11Ni yule yule Roho mumoja anayetenda mambo hayo yote, akimupa kila mumoja zawadi mbalimbali kama anavyopenda.
Mwili mumoja una viungo vingi12Kwa maana, Kristo ni kama mwili mumoja unaokuwa na viungo vingi. Ijapokuwa viungo vya mwili ni vingi, vinakuwa mwili mumoja tu.
13Vilevile sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, watumwa na watu wanaokuwa huru, tumebatizwa kwa Roho mumoja kusudi tukuwe mwili mumoja na sisi wote tumekunyweshwa Roho mumoja.
14Mwili hauundwi na kiungo kimoja tu, lakini na viungo vingi.
15Kama muguu ungesema: “Kwa sababu mimi si mukono, basi mimi si wa mwili,” hata vile haungeacha kuwa kiungo cha mwili.
16Na kama sikio lingesema: “Kwa sababu mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hata vile halingeacha kuwa kiungo cha mwili.
17Kama mwili wote ungekuwa jicho, namna gani ungeweza kusikia? Na kama ungekuwa sikio, namna gani ungeweza kunusa?
18Lakini sasa, Mungu amepanga viungo vya mwili kila kimoja kama ilivyomupendeza.
19Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili haungekuwa!
20Kwa hivi sasa kunakuwa viungo vingi lakini mwili ni mumoja.
21Jicho haliwezi kuuambia mukono: “Sina lazima yako!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: “Sina lazima yenu!”
22Lakini zaidi ya hiyo, viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa zaifu, ndivyo vinavyokuwa vya lazima.
23Tena viungo vile tunavyozania kwamba havistahili heshima kubwa ndivyo tunavyoheshimu zaidi. Na viungo vinavyokuwa vya haya ndivyo tunavyotunza sana,
24wakati vile vinavyoheshimiwa havihitaji kitu. Mungu ameunganisha mwili hata akavipatia heshima zaidi viungo vilivyokosa heshima,
25kusudi kusikuwe mabishano katikati ya viungo vya mwili, lakini vyote visaidiane sawasawa.
26Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.
27Ninyi wote ni mwili wa Kristo, na kila mumoja wenu ni kiungo cha mwili ule.
28Vilevile Mungu ameweka kwanza mitume katika kanisa; pili manabii na tatu walimu; kisha kunakuwa wale wenye zawadi ya kufanya miujiza, ya kuponyesha wagonjwa, ya kusaidia wengine, ya kuongoza wengine, ya kusema luga za ajabu.
29Wote si mitume, manabii au walimu. Wote hawana uwezo wa kufanya miujiza,
30wa kuponyesha wagonjwa, wa kusema kwa luga za ajabu, au wa kutafsiri.
31Basi mutamani sana zawadi inayokuwa bora zaidi.
Lakini sasa, nitawaonyesha njia nzuri sana kuliko zote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.