1Katika nyakati hizo, mifupa ya wafalme wa Yuda, mifupa ya wakubwa wao, mifupa ya makuhani, mifupa ya manabii na mifupa ya wakaaji wote wa Yerusalema itachimbuliwa toka ndani ya makaburi yao.
2Itaachwa imetandazwa mbele ya jua na mwezi na nyota zote za mbingu, vitu ambavyo walivyopenda na kuvitumikia, na kuviendea kwa kuuliza shauri na kuviabudu. Mifupa hiyo haitakusanywa wala kuzikwa, lakini itabaki kama vile mboleo juu ya udongo.
3Watu wote watakaobaki wa jamaa hii mbaya, pahali popote pale nilipowasambaza, wataona heri kufa kuliko kuishi.
–Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.
Zambi na azabu ya watu wa Yerusalema4Wewe Yeremia utawaambia kwamba:
Yawe anasema hivi:
Mutu akianguka, hasimami tena?
Mutu akipotea, harudii tena katika njia yake?
5Mbona basi, watu hawa wameacha njia inayokuwa sawa
na kuendelea katika upotovu wao?
Wanashikamana na miungu yao ya uongo,
na kukataa kunirudilia mimi!
6Mimi nilisikiliza kwa uangalifu,
lakini wao hawakusema ukweli wowote.
Hakuna mutu anayetubu uovu wake,
wala kujiuliza hivi: Nimefanya nini?
Kila mumoja wao anashika njia yake,
kama farasi anavyokimbia haraka kwa vita.
7Hata korongo anajua wakati wa kuhama;
njiwa, mbaruwayi na koikoi,
wanajua nyakati zao za kurudi.
Lakini hawa watu wangu hawajui
maagizo ya Yawe.
8Ninyi munajidai kwamba muko na hekima,
nanyi munafuata amri zangu mimi Yawe.
Lakini kalamu ya uongo ya waandishi
imeifanya kuwa uongo.
9Wenye hekima kati yenu wanafezeheka,
watahangaishwa na kunaswa.
Wamelikataa neno la Yawe.
Basi ni hekima gani wanayokuwa nayo?
10Kwa hiyo, wake zao nitawatoa kwa waume wengine,
nayo mashamba yao nitawapa wengine.
Maana, tangu mudogo mpaka mukubwa,
kila mumoja ana tamaa ya faida isiyokuwa ya haki.
Tangu manabii mpaka makuhani,
kila mumoja anatenda kwa udanganyifu.
11Wanatunza vidonda vya watu wangu juujuu,
wakisema: “Kuna amani, kuna amani”,
ingawa hakuna amani yoyote!
12Walisikia haya walipotenda machukizo hayo?
Hapana, hawakusikia haya hata kidogo.
Hata zamiri hazikuwagonga.
Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka;
nitakapowaazibu, wataangamia.
–Ni Yawe anayesema hivyo.
13Nilitaka kuchuma matunda kutoka kwao.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Lakini sikupata zabibu hata moja juu ya muzabibu,
sikupata tini zozote juu ya muti wa tini;
hata majani yao yamekauka.
Hata nilichokuwa nimewapa kimetoweka.
14Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa?
Tukusanyike, tuingie katika miji yenye kuzungukwa na kuta,
tuangamie kule!
Yawe, Mungu wetu, amekusudia tuangamie,
ametupa maji yenye sumu tukunywe,
kwa sababu tumemukosea yeye.
15Tulitazamia kupata amani
lakini hakuna kitu kizuri.
Tulitazamia kupona
lakini tumepatwa na vitisho.
16Kelele za farasi wa waadui zinasikilika tokea Dani,
kwa mulio wa farasi wao wa vita,
inchi nzima inatetemeka.
Wanafika na kuharibu inchi na vyote vinavyokuwa ndani yake,
kuangamiza muji pamoja na wote wanaokaa humo.
17Basi nitawatumia ninyi nyoka;
nyoka wenye sumu wasioweza kulogwa na walozi,
nao watawauma ninyi.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Huzuni ya Yeremia18Huzuni yangu haiwezi kutulizwa,
moyo wangu unaugua ndani yangu.
19Sikiliza kilio cha watu wangu,
kutoka kila upande katika inchi.
Yawe hayuko tena katika Sayuni?
Mufalme wa Sayuni hayuko tena?
Lakini Yawe anasema:
Mbona wamenikasirikisha na sanamu zao za kuchongwa,
nayo miungu yao ya kigeni?
20Wakati wa mavuno umepita,
nao wakati wa jua kali umekwisha,
nasi hatujaokolewa!
21Mimi ninavunjika moyo,
ninaomboleza na kufazaika,
kwa sababu watu wangu wameumizwa sana.
22Hakuna dawa ya kupakaa kule Gileadi?
Hakuna muganga kule?
Mbona basi watu wangu hawajaponyeshwa?
23Heri kichwa changu kingekuwa kisima cha maji,
na macho yangekuwa chemichemi ya machozi
kusudi nipate kulia muchana na usiku,
kwa ajili ya watu wangu waliouawa!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.