Ezekieli 47 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Chemichemi inayotoka katika hekalu

1Yule mutu akanirudisha kwenye kiingilio cha hekalu. Huko, maji yalikuwa yakitoka chini ya kizingiti cha hekalu kuelekea upande wa mashariki, (kwa maana hekalu lilielekea upande wa mashariki). Maji yalikuwa yakitiririka kutoka chini ya upande wa kusini wa mulango wa hekalu, upande wa kusini wa mazabahu.

13Bwana wetu Yawe anasema hivi: Hii ndiyo mipaka ya inchi mutakayoigawanyia makabila kumi na mawili ya Waisraeli. Lakini kabila la Yosefu lipewe mara mbili.

14Ninyi wote mutagawanyana sawa. Niliapa kuwa nitawapa babu zenu inchi hii, nayo itakuwa mali yenu.

15Upande wa kaskazini mupaka utapita kutoka bahari ya Mediteranea, kuelekea muji wa Hetiloni, hata pahali pa kuingia Hamati na kuendelea mpaka Zedada.

16Kutoka hapo utaendelea mpaka Berota na Sibraimu (unaokuwa kati ya Damasiki na Hamati), na mpaka muji wa Hazori-Hatikoni unaokuwa katika inchi ya Haurani.

17Hivyo mupaka utakwenda kutokea bahari ya Mediteranea kuelekea mashariki mpaka katika muji wa Hazorenoni ukipakana na maeneo ya Damasiki na Hamati kwa upande wa kaskazini.

18Upande wa mashariki, mupaka utakuwa muto Yordani unaoelekea kati ya Haurani na Damasiki, Gileadi na inchi ya Israeli. Vilevile mupaka utapitia upande wa mashariki wa bahari ya Chumvi mpaka Tamari.

19Upande wa kusini, toka Tamari mupaka utaendelea mpaka kwenye chemichemi ya Meriba-Kadesi. Kutoka Meriba-Kadesi mupaka utaelekea kusini magaribi mpaka bahari ya Mediteranea ukipitia upande wa mashariki ya inchi ya Misri.

20Upande wa magaribi, mupaka ni bahari ya Mediteranea na utapanda upande wa kaskazini mpaka pahali pa kuingilia Hamati.

21Basi, mutagawanya inchi hii kati yenu kulingana na makabila ya Waisraeli.

22Mutaigawanya kuwa mali yenu. Wageni watakaokaa kati yenu, wale watakaozalia watoto kati yenu, wapewe vilevile sehemu ya inchi munapoigawanya. Hao wanapaswa kutendewa kama wanainchi wa Israeli na wana haki ya kupiga kura kwa kupata sehemu ya inchi pamoja na makabila ya Waisraeli.

23Kila mugeni anayekaa nanyi atapewa sehemu yake pamoja na watu wa kabila ambamo anaishi.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help