Zaburi 111 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu anasifiwa kwa matendo yake

1Haleluia!

Nitamushukuru Yawe kwa moyo wangu wote,

katika mukutano wa watu wa usawa.

2Matendo ya Yawe ni makubwa sana!

Wote wanaoyafurahia wanayachunguza.

3Kila anachofanya kimejaa utukufu na heshima;

haki yake inadumu milele.

4Amesababisha matendo yake ya ajabu yakumbukwe;

Yawe ni mwenye huruma na rehema.

5Anawapa chakula wenye kumwabudu;

hasahau hata kidogo agano lake.

6Amewaonyesha watu wake nguvu ya matendo yake,

amewapa inchi za mataifa mengine zikuwe mali yao.

7Matendo yake ni ya haki na ya kuaminika;

kanuni zake zote ni za kutegemewa siku zote.

8Amri zake zinadumu milele;

zimetolewa kwa uaminifu na usawa.

9Aliwakomboa watu wake

na kufanya nao agano la milele.

Yeye ni mutakatifu na wa kutisha sana!

10Kumwogopa Yawe ni musingi wa hekima;

wote wanaotii amri zake wanajaliwa akili.

Sifa zake zinadumu milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help