Ufunuo 15 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wamalaika saba na mapigo ya mwisho

1Kisha nikaona tena katika mbingu kitambulisho kingine kikubwa na cha kushangaza sana. Kulikuwa wamalaika saba wanaoshika mapigo saba. Mapigo haya ndiyo yaliyokuwa ya mwisho, kwa maana ni yale Mungu atakayotumia kwa kutimiza kasirani yake.

2Tena nikaona kitu kinachofanana na bahari ya kioo, iliyochanganyika na moto. Nikaona vilevile wale walioshinda yule nyama wa ajabu pamoja na sanamu yake na tarakimu zinazolingana na herufi za jina lake. Watu wale walikuwa wakisimama juu ya ile bahari ya kioo wakishika vinubi walivyopewa na Mungu.

3Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema:

“Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo,

matendo yako ni makubwa na ya ajabu!

Ewe Mufalme wa mataifa,

kazi zako ni za haki na za kweli!

4Ewe Bwana, hakuna asiyekuogopa,

wala hakuna asiyekutukuza,

kwa maana wewe peke yako ndiwe mutakatifu.

Mataifa yote yatakuja kukuabudu,

kwa maana matendo yako ya haki yameonyeshwa wazi.”

5Na nyuma ya pale nikaona hekalu limefunguliwa mbinguni; mule mulikuwa hema yenye vibao vya agano la Mungu.

6Na wale wamalaika saba walioshika mapigo saba wakatoka katika lile hekalu. Walikuwa wamevaa nguo zilizofumwa na nyuzi za pamba zenye kungaa na mikaba ya zahabu katika viuno vyao.

7Na mumoja wa vile viumbe vine vya ajabu akawapa wale wamalaika saba vikombe saba vya zahabu vyenye kujaa kasirani ya Mungu, anayeishi kwa milele.

8Hekalu likajaa moshi kutokana na utukufu wa Mungu na uwezo wake. Na hakuna mutu aliyeweza kuingia ndani ya hekalu mpaka yale mapigo yaliyoletwa na wale wamalaika saba yalipotimizwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help