1 Watesalonika 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Salamu

1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa Silvano na Timoteo. Tunawaandikia ninyi kanisa la Tesalonika munaoungana na Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo. Tunawatakia neema na amani.

Maisha ya imani ya Watesalonika

2Tunamushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wote. Nasi tunawakumbuka katika maombi yetu bila kuchoka.

3Kwa maana tunakumbuka mbele ya Mungu Baba yetu namna munavyotumika kwa imani na munavyojisumbua na kazi kwa ajili ya upendo wenu. Vilevile tunakumbuka namna tumaini lenu katika Yesu Kristo linavyokuwa imara.

4Wandugu wapendwa wa Mungu, tunajua kwamba yeye amewachagua kuwa watu wake.

5Kwa maana tulipohubiri Habari Njema kwenu, hatukuihubiri kwa maneno tu, lakini kwa uwezo na kwa musaada wa Roho Mutakatifu na kwa uhakika kabisa. Munajua namna gani tulivyoishi katikati yenu, kusudi tupate kuwafalia.

6Ninyi mumefuata mufano wetu na mufano wa Bwana, kwa kuwa ingawa muliteswa sana, mulipokea neno la Mungu kwa furaha inayotoka kwa Roho Mutakatifu.

7Kwa njia hii mumeonyesha mufano muzuri kwa waamini wote wa Makedonia na Akaya.

8Kwa maana tokea kwenu neno la Bwana lilienea, si katika Makedonia na Akaya tu, lakini habari za imani kwa Mungu zilisambaa fasi zote, hata sisi hatukukuwa tena na lazima ya kusema neno juu ya ile.

9Wao wenyewe wanaeleza namna mulivyotupokea wakati tulipofika kwenu na namna mulivyoacha kuabudu sanamu na kumurudilia Mungu. Mulifanya vile kusudi mumutumikie Mungu mwenye uzima na wa kweli

10na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help