Isaya 12 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wimbo wa shukrani

1Siku hiyo mutasema:

Ninakushukuru, ee Yawe,

maana ingawa ulinikasirikia,

hasira yako imetoweka,

nawe umenifariji.

2Mungu ndiye mwenye kuniokoa,

nitamutegemea yeye, wala sitaogopa;

Yawe ananijalia nguvu;

yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.

3Mutachota maji kwa furaha

kutoka visima vya wokovu.

4Siku hiyo mutasema:

Mumushukuru Yawe,

muombe kwa jina lake.

Mujulishe kwa mataifa matendo yake,

mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa.

5Mumwimbie Yawe sifa

maana ametenda mambo makubwa;

haya yajulikane katika dunia yote.

6Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha,

enyi wakaaji wa Sayuni,

maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help