1Siku ya kwanza ya mwezi wa tatu tangu walipotoka katika inchi ya Misri, watu wa Israeli wakafika katika jangwa la Sinai.
2Walipoondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, kule wakapiga kambi mbele ya mulima Sinai.
3Basi, Musa akapanda juu kwenye mulima kwa Mungu.
Halafu Yawe akamwita Musa kutoka kule juu ya mulima, akamwambia: “Hivi ndivyo utakavyowaambia wazao wa Yakobo, wale Waisraeli:
4‘Ninyi wenyewe mumeona jinsi nilivyowatendea Wamisri na jinsi nilivyowapeleka ninyi kama vile tai anavyopeleka watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu.
5Sasa basi, kama mukitii sauti yangu na kushika agano langu, mutakuwa watu wangu wachaguliwa kati ya mataifa yote, maana dunia yote ni yangu.
7Basi, Musa akarudi, akawakusanya pamoja wazee wa Waisraeli na kuwaambia maneno hayo aliyoamuriwa na Yawe.
8Watu wote wakaitikia kwa pamoja wakisema: “Mambo yote Yawe aliyosema, tutayafanya.” Musa akamujulisha Yawe jibu lile la watu.
9Yawe akamwambia Musa: “Basi, mimi nitakufikia katika wingu zito kusudi Waisraeli wapate kunisikia ninaposema nawe na kukuamini siku zote.”
Kisha Musa akamwambia Mungu jinsi watu walivyosema.
10Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Uwaambie wafue nguo zao
11wakuwe tayari kwa kesho kutwa, maana siku hiyo ya tatu mimi Yawe nitashuka juu ya mulima Sinai mbele ya watu wote.
12Tena wewe utawawekea watu mupaka kuzunguka mulima kuwaambia wajilinde sana wasipande juu kwenye mulima wala kugusa mupaka wake. Yeyote atakayegusa mulima, atauawa. Ang. Ebr 12.18-20
13Mutu asimuguse mutu yule. Atauawa kwa kupigwa mawe au mushale. Akuwe ni mutu au ni nyama, hataishi. Wakati baragumu itakapopigwa mufululizo, watu wote watakaribia mulima.”
14Basi, Musa akashuka toka juu ya mulima na kuwaendea watu, akawatakasa, nao wakafua nguo zao.
15Kisha akawaambia watu wote: “Kesho kutwa mukuwe tayari na mwanaume yeyote asimukaribie mwanamuke.”
16Basi, siku ya tatu asubui, kukatokea ngurumo na umeme na wingu zito juu ya mulima. Kukasikilika vilevile sauti kubwa ya baragumu ambayo iliwatetemesha watu wote katika kambi. Ang. Ufu 4.5 Ang. Kumb 4.11-12
17Kisha Musa akawaongoza watu wote kutoka katika kambi, wakaenda kukutana na Mungu. Wote walikwenda wakajipanga chini ya mulima.
18Mulima wa Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi kwa sababu Yawe alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto ule ulipanda juu kama moshi wa furu kubwa na mulima wote ukatetemeka kwa nguvu.
19Sauti ya baragumu ikazidi kuongezeka na Musa akaongea na Mungu. Mungu naye akamujibu katika ngurumo.
20Yawe akashuka juu ya mulima Sinai, akamwita Musa kutoka kule juu, naye Musa akapanda juu ya mulima.
21Kisha Yawe akamwambia Musa: “Shuka chini uwaonye watu wote wasikuje kuniona. Kama sivyo wengi wao wataangamia.
22Hata makuhani ambao wananikaribia wanapaswa kujitakasa, kama sivyo nitawaazibu.”
23Musa akamwambia Yawe: “Watu hawa hawawezi kupanda juu ya mulima wa Sinai maana wewe mwenyewe ulituamuru tuweke mupaka kuzunguka mulima na kuutakasa.”
24Yawe akasema: “Teremuka chini kisha urudi pamoja na Haruni. Lakini usiwaruhusu makuhani na watu wengine wapite mupaka na kuja kwangu, kama sivyo nitawaazibu.”
25Basi, Musa akashuka na kuwaambia Waisraeli mambo yote aliyoagizwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.