1Haleluia!
Musifu jina la Yawe,
mumusifu, enyi watumishi wake.
2Mumusifu, enyi munaokaa katika nyumba yake,
ndani ya viwanja vya nyumba ya Mungu wetu!
3Mumusifu Yawe kwa sababu yeye ni muzuri;
mumutukuze kwa nyimbo, maana inafaa.
4Yawe amemuchagua Yakobo kuwa wake,
watu wa Israeli kuwa mali yake mwenyewe.
5Ninajua hakika kwamba Yawe ni mukubwa;
Bwana wetu ni mukubwa kupita miungu yote.
6Yawe anafanya chochote anachotaka,
mbinguni, katika dunia, ndani ya bahari na shimo ndefu.
7Analeta mawingu kutoka miisho ya dunia,
anapiga umeme na kunyesha mvua,
anavumisha upepo kutoka gala zake.
8Aliwaua wazaliwa wa kwanza huko Misri,
wazaliwa wa watu na wa nyama vilevile.
9Alifanya miujiza na maajabu kwako, ee Misri,
mufalme wa Misri na wakubwa wake wote.
10Aliangamiza mataifa mengi,
akawaua wafalme wenye nguvu
11kama vile Sihoni mufalme wa Waamori,
Ogi mufalme wa Basani,
na wafalme wote wa Kanana.
12Alikamata inchi zao kuwa urizi wa watu wake;
zikuwe urizi wa watu wake Israeli.
13Jina lako, ee Yawe, linadumu milele,
utakumbukwa nyakati zote.
14Yawe atawatetea watu wake;
na kuwaonea huruma watumishi wake.
15Miungu ya uongo ya mataifa ni feza na zahabu,
imetengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16Ina vinywa, lakini haisemi;
ina macho, lakini haioni.
17Ina masikio, lakini haisikii;
wala haiwezi hata kuvuta pumzi.
18Wote walioifanya wafanane nayo,
kila mumoja anayeitegemea!
19Enyi watu wa Israeli, mumutukuze Yawe!
Enyi makuhani, mumutukuze Yawe!
20Enyi Walawi, mumutukuze Yawe!
Enyi munaomwabudu Yawe, mumutukuze!
21Atukuzwe Yawe katika Sayuni,
atukuzwe katika makao yake Yerusalema.
Haleluia!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.