Waebrania 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wokovu mukubwa

1Kwa sababu hiyo, tunapaswa kushikamana zaidi na habari tuliyosikia, kusudi tusipotee mbali.

2Ujumbe wa Sheria uliotangazwa na malaika ulitimizwa, na hata kila mutu aliyekosa kuufuata na kuasi aliazibiwa sawa inavyostahili.

3Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.

4Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.

Mwongozi wa wokovu

5Mungu hakuwapa wamalaika uwezo wa kutawala ulimwengu unaokuja, ndio ule tunaosema juu yake.

6Tena maneno haya yanahakikishwa na pahali pengine katika Maandiko Matakatifu:

“Mutu ni nini hata umukumbuke,

mwanadamu ni nini hata umushugulikie?

7Umemufanya kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika.

Umemujaza utukufu na heshima.

8Umemupa mamlaka juu ya vitu vyote.”

Wakati inaposemwa ya kama Mungu amemupa mutu mamlaka juu ya vitu vyote, maana yake hakuacha hata kitu kimoja. Ingawa hivi, hata sasa hatuoni kwamba amepewa mamlaka juu ya vitu vyote.

9Lakini mambo tunayoona ndiyo haya: Yesu alifanywa kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika kusudi kwa neema ya Mungu, Yesu akufe kwa ajili ya watu wote. Na sasa kwa njia ya kile kifo kilichomufikia, amepata utukufu na heshima.

10Kwa hiyo ilifaa kwamba Mungu aliyeumba vitu vyote na kuvilinda imara, amufanye Yesu kuwa mukamilifu kwa njia ya mateso, kusudi awalete watoto wengi kuwa washiriki wa utukufu wa Mungu. Kwa maana Yesu ndiye anayewaongoza watu wapate kuokoka.

11Yeye anawatakasa watu toka katika zambi, na wale wanaotakaswa naye, wote ni watoto wa Baba mumoja. Ni kwa sababu hiyo Yesu hasikii haya ya kuwaita wandugu zake.

12Kwa maana anasema:

“Ee Mungu, nitatangaza jina lako kwa wandugu zangu,

nitakusifu katikati ya mukutano.”

13Tena anasema:

“Nitamutumainia Mungu.”

Na tena anasema:

“Mimi ni hapa pamoja na watoto Mungu alionipatia.”

14Basi kwa kuwa hao watoto ni wanadamu, wenye mwili na damu, Yesu vilevile alitwaa ile hali ya mwanadamu. Alifanya hivi kusudi kwa njia ya kufa kwake amwangamize Shetani aliyekuwa na uwezo wa kuleta lufu.

15Vilevile aliwafungua wale wote walioishi kama watumwa katika maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa lufu.

16Kwa maana hakika hakukuja kuwasaidia wamalaika, lakini alikuja kuwasaidia wazao wa Abrahamu.

17Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.

18Na kwa sababu yeye mwenyewe alijaribiwa na kuteswa, anaweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help