1Waisraeli wote wakasafiri toka Elimu na kufika katika jangwa la Sini kati ya Elimu na Sinai. Hii ilikuwa siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili tangu walipoondoka inchi ya Misri.
2Basi, Waisraeli wote pamoja wakamunungunikia Musa na Haruni kule katika jangwa. Wakasema hivi:
3“Heri Yawe angelituua tulipokuwa katika inchi ya Misri ambako tulikaa, tukakula nyama na mikate hata tukashiba. Lakini ninyi mumetuleta huku katika jangwa kwa kuua jamii hii yote kwa njaa!”
4Halafu Yawe akamwambia Musa: “Mimi nitawanyeshea mikate kutoka mbinguni. Kila siku watu watatoka na kukusanya chakula cha siku hiyo. Kwa njia hii nitawapima nione kama watafuata sheria zangu au hawatazifuata. Hawakujua kilikuwa kitu gani.
Basi, Musa akawaambia: “Huu ni mukate ambao Yawe amewapa mukule. kwa kila mutu katika hema yake.”
17Basi, Waisraeli wakafanya hivyo na ikakuwa kwamba wengine waliokota kwa wingi na wengine kidogo.
18Lakini wote walipopima kiasi walichookota katika kipimo cha litre ine, walitambua kwamba aliyeokota kingi hakukuwa na cha zaidi na aliyeokota kidogo, hakupungukiwa. Kila mumoja alikuwa ameokota kiasi alichoweza kula.
19Musa akawaambia watu: “Mutu yeyote asiache chakula hicho mpaka asubui.”
20Lakini watu hawakumusikiliza Musa. Wamoja kati yao walijiwekea chakula mpaka asubui. Lakini asubui chakula hicho kikakuwa kimeoza na kuwa na vidudu. Musa akawakasirikia sana watu.
21Basi, kila asubui walikusanya chakula kila mutu kipimo alichohitaji kula. Jua lilipopanda juu na kuwa kali, kile chakula kingine kiliyeyuka.
22Katika siku ya sita, Waisraeli walikusanya chakula hicho mara mbili, vipimo viwili vya litre ine kwa kila mutu. Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea Musa, wakamwelezea jambo hilo.
23Musa akawaambia: “Hii ndiyo amri ya Yawe. Kesho ni siku ya mapumziko. Ni Sabato takatifu ya Yawe. Basi, muende mupike au kuchemusha kile chakula munachohitaji leo na chakula kitakachobakia mukiweke mpaka kesho.” Kilikuwa kama mbegu za mutama mweupe na onjo yake ilikuwa kama mukate mwembamba uliotiwa asali.
34Basi, Haruni aliweka mana Pahali Patakatifu mbele ya Sunduku la Agano kusudi ilindwe kama vile Yawe alivyomwagiza Musa.
35Waisraeli walikula mana kwa muda wa miaka makumi ine, mpaka walipofika katika inchi iliyofaa kwa kuishi, ni kusema mpaka walipovuka mupaka wa Kanana. Ang. Yos 5.12
36(Posho ya mana ilikuwa sehemu ya kumi ya kipimo cha kawaida kinachoitwa efa.)
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.