1Tunawaandikia ninyi juu ya Neno la uzima, lililokuwa tangia mwanzo. Sisi tulilisikia, tuliliona kwa macho yetu wenyewe, tuliliangalia na kuligusa kwa mikono yetu wenyewe.
2Uzima huu ulipotokea, sisi tuliuona. Kwa sababu hii tunaushuhudia na kuwatangazia habari za huo uzima wa milele, uliokuwa pamoja na Baba na ulioonyeshwa kwetu.
3Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.
4Tunawaandikia ninyi maneno haya kusudi tupate kujazwa na furaha kabisa.
Mungu ni mwangaza5Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kutoka kwa Yesu Kristo na kuitangaza kwenu: Mungu ni mwangaza, na ndani yake hamuna giza hata kidogo.
6Tukisema kwamba tunashirikiana naye, lakini tunaishi katika giza, tunasema uongo, nayo matendo yetu si ya kweli.
7Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.
8Tukisema kwamba hatuna zambi, tunajidanganya sisi wenyewe, wala ukweli hauko ndani yetu.
9Lakini tukiitikia zambi zetu mbele ya Mungu, yeye atatusamehe zambi zetu na kutusafisha toka katika maovu yote kwa maana yeye ni mwaminifu na mwenye haki.
10Tukisema kwamba hatukutenda zambi, tunamugeuza Mungu kuwa mwongo, na ukweli wa neno lake si ndani yetu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.